Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Tuesday, May 31, 2011

NGAO YA MALKIA WA UINGEREZA YAPATIKANA YANGA

Ngao ya Malkia wa Uingereza iliyoshindaniwa Mwaka 1953

Uongozi wa Klabu ya Yanga umefanikiwa kupata Ngao mbili zenye hadhi ya kimataifa ikiwemo ngao ya Malkia Elizaberth wa Uingereza iliyopatikana Mwaka 1953 na nyingine iliyoshindaniwa katika miaka ya 1954.Taarifa hiyo imetolewa leo na Katibu Mkuu wa Klabu ya Yanga Celestine Mwesigwa ambaye Ngao hizo ni hazina ya Klabu ya Yanga katika kuweka kumbukumbu ya Yanga ikiwemo na vitu vingine.“Baada ya kupata Ngao hizi ipo haja ya kuwatafuta wazee waliowahi kuiongoza Klabu yetu ama waliocheza ili tuweze kupata uhakika na Ngao hizi tulizozipata.”Mwesigwa.

Katibu Mkuu ametoa wito kwa wanachama na wadau wote wa Yanga kujitokeza kwa wingi kama kuna mtu ana taarifa yoyote kuhusu Ngao hizo pamoja na zawadi mbalimbali ambazo watu wanazo majumbani kwao kuvirejesha mara moja katika Makao Makuu ya Klabu ya Yanga.

Hivi karibuni uongozi wa Yanga umeonyesha nia ya kuweka mikakati ya kuanzishwa eneo la kutunzia kumbukumbu mbalimbali za Klabu ya Yanga vikiwemo Vikombe mbalimbali,Ngao pamoja na tuzo za wachezaji na viongozi.

No comments :

Post a Comment