Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Tuesday, May 24, 2011

MISS LINDI 2011 KUPATIKANA JUNI 4

Na Dina Ismail


SHINDANO la kumtafuta Miss Lindi mwaka 2011 linatarajiwa kufanyika juni 4 mwaka huu katika kumbi wa hoteli ya Lindi Oceanic mkoani Lindi,imefahamika.
Mratibu wa shindano hilo lililoandaliwa na kampuni ya Alliance Entertainment Shah Ramadhan alisema mpaka sasa warembo tisa wamejitokeza kwa ajili ya kushiriki shindano hilo na kusema kuwa milango bado ipo wazi kwa wasichana wenye sifa kujitokeza.
Alisema warembo watakaoshiriki wanatarajiwa kuanza kujinoa Mei 29 katika ukumbi huo huku mkufunzi aliyebobea katika masuala hayo Caroline Zayumba akitarajiwa kuendesha zoezi hilo.
.”Kwa kweli tumejipanga kuhakikisha tunatoa mrembo ambaye atarudisha hadhi ya mkoa wa Lindi kama miaka iliyopita, warembo tulionao wote ni bomba, pia tunaomba wadhamini wajitokeze kwa wingi kutusaidia”, Alisema.
Mratibu huyo alisema mpaka sasa makampuni yaliyojitokeza kudhamini ni pamoja na Vodacom, Ndanda Spring Water, Muhsin General Enteroprises, Live Trading Center, Pride Fm na Lindi Oceanic hotel.
Taji la Miss Lindi linashikiliwa na Mary Adam pichani kushoto

No comments :

Post a Comment