Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Tuesday, May 24, 2011

Mada Maugo Na Francis Cheka Kumaliza Ubishi Idd Pili



Mratibu wa pambano hilo Kaike Siraju


Mabondia Mada Maugo (kushoto) na Francis Cheka Kulia, katikati ni Mratibu wa Pambano la wakali hao Kaike Siraju
MABONDIA Francis Cheka na Mada Maugo wanatarajia kupanda ulingoni ka mapambano mkali siku ya Idd Pili kwa ajili ya kumaliza ubishi wa nani mbabe dhidi ya mwenzake, katika pambano la kuwania ubingwa wa Mabara (UBO) linalotarajiwa kupigwa katika Uwanja wa Jamhuri, mkoani Morogoro.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, mratibu wa pambano hilo, Kaike Siraju, alisema, tayari mabondia hao wameshasaini mkataba wa kucheza pambano hilo la raundi 10 uzito wa Kati, kilo 72.5
Cheka na Maugo wanacheza pambano hilo ikiwa ni miezi kadhaa baada ya mabondia hao kuzichapa Januari Mosi mwaka huu katika Ukumbi wa (PTA) na Cheka kuibuka mbabe kwa ushindi wa pointi moja, hali iliyozua malumbano kuwa majaji walimpendelea bondia huyo.
Alisema, pambano hilo litapambwa na mapambano mengine ya utangulizi, ambako Maliki Kinyogoli atazichapa na Deo Njiku raundi 10 uzito wa (Superfly), Seba Temba na Obote Ameme huku Fadhili Majiha akimvaa Sadick Abdul-Aziz raundi sita.
Mapambano mengine yatawakutanisha Doi Miyeyusho na Albert Mbena huku Cosmas Cheka akivurumishana masumbwi na Hoseni Mbonde.

No comments :

Post a Comment