Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Sunday, May 8, 2011

VODACOM FOUNDATION YATOA MSAADA WA MADAWATI 50 KWA SHULE YA MSINGI UNUNIO



Ofisa Elimu wa kata ya kunduchi, Geradine Ishengoma ,akiwasisitiza jambo baadhi ya wanafunzi wa shule ya msingi Ununio kutunza madawati 50 yenye thamani ya zaidi ya shilingi million 4 baada ya kukabidhiwa ba msaada na Vodacom Foundation na Ofisa wa mfuko huo Grace Lyon (kulia).

Ofisa wa mfuko wa kusaidia jamii wa Vodacom, (Vodacom Foundation) Grace Lyon, akifurahi na baadhi ya mwanafunzi wa darasa la kwanza Jamila Hamis wa shule ya msingi ununio iliyopo kata ya kunduchi wilaya Kinondoni jijini Dares Salaam baada ya kukabidhi madawadi 50 yenye thamani ya zaidi ya shilingi million 4,wengine ni baadhi ya wanafunzi wa shule hiyo.
Baadhi ya wanafunzi wa shule ya msingi Ununio iliyopo Kata ya Kunduchi wilaya ya Kinondoni jijini Dares Salaam wakifurahia msaada wa madawati 50 yaliyotolewa na Vodacom Foundation yenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 4 na kukabidhiwa na Afisa wa mfuko huo, Grace Lyon hayupo pichani.



Baadhi ya wanafunzi wa shule ya msingi Ununio iliyopo kata ya kunduchi Wilaya ya Kinondoni wakisikiliza jambo kwa umakini kutoka kwa Mtaalamu wa mambo ya habari wa Vodacom Tanzania Matina Nkurlu,baada ya kukabidhiwa msaada wa madawati 50 yenye ya zaidi ya Shilingi million 4.

No comments :

Post a Comment