Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Tuesday, February 21, 2012

Tamasha lahamishiwa Dodoma badala ya Mwanza







MWENYEKITI wa Tamasha la Pasaka, Alex Msama amesema kuwa, tamasha hilo limepangwa kufanyika Aprili 9, katika Uwanja wa Jamhuri mkoani Dodoma.

Akizungumza jijini leo, Msama alisema kuwa, kamati imeamua kulihamishia tamasha hilo mkoani Dodoma badala ya Mwanza, baada ya kuridhika na maombi ya wadau wa muziki huo.

"Kamati kazi yake kubwa ni kupokea maoni kutoka kwa wadau na kuyafanyia kazi, wajumbe wameamua lifanyike mkoani Dodoma badala ya Mwanza," alisema.

Mwenyekiti huyo alisema kuwa, awali tamasha hilo lilipangwa kufanyika mkoani Mwanza, kwenye Uwanja wa CCM Kirumba Aprili 9, mwaka huu.

"Ni kitu cha kawaida kuhamisha sehemu moja kwenda sehemu nyingine, maamuzi ya kamati ni ya kuyaheshimu," alisema.

Mwaka jana, tamasha hilo lilifanyika katika mikoa mitatu, Dar es Salaam, Dodoma na Mwanza.

Pia, Msama alisema kutokana na tamasha hilo kuwa la kimataifa, amewataka wafanyabiasha kujitokeza kudhamini tamasha hilo kubwa nchini.

Mpaka sasa, baadhi ya waimbaji nyota wa ndani na nje ya nchi wamethibitisha kushiriki, lakini kwa sasa wanaendelea na taratibu za kupata kibali cha kufanya kazi.

"Tayari baadhi ya waimbaji nyota wa ndani na nje waliopelekewa mialiko, wamethibitisha kushiriki, kilichobaki ni kushughulishia vibali vyao," alisema.

"Bado tunapokea maoni kutoka kwa wadau wetu, tunaomba mzidi kututumia ili tuyafanyie kazi kabla ya tarehe ya tamasha hilo," alisema.

Tamasha la Pasaka mwaka huu litafanyika Aprili 8, mwaka huu jijini Dar es Salaam na Aprili 9 litafanyika mkoani Dodoma. Kwa hisani ya blog ya majuto balile

No comments :

Post a Comment