Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Wednesday, April 10, 2013

Filamu ya After Death kutolewa hadharani Mei






FILAMU maalum kwa ajili ya kumuenzi marehemu Steven Kanumba iitwayo 'After Death' iliyozunduliwa kwa kishindo wakati wa hafla ya 'Kanumba Day' inatarajiwa kuachiwa rasmi mwezi ujao.
Kwa mujibu wa waandaaji, filamu hiyo itatoka Mei kwa lengo la kutoa fursa ya kazi mpya ya marehemu Kanumba ya 'Love & Power' iliyozinduliwa pamoja Aprili 7 kwenye viwanja vya Leaders itambe sokoni ikitarajiwa kuachiwa rasmi sokoni Ijumaa hii.
Muongozaji wa filamu hiyo ilitungwa na Jacklyne Wolper, Leah Richard 'Lamata', alisema licha ya mashabiki waliofika Leaders kushuhudia uzinduzi wa filamu hizo kuitaka kuinunua, walikwama kwa vile muda wake wa kuitoa bado.
Lamata alisema mashabiki hao wanapaswa kuwa na subira mpaka mwezi ujao kazi hiyo itakapoachiwa rasmi kulingana na ratiba iliyopo.
"Tunashukuru tumefanikiwa kuwaonjesha ladha na kupokewa vyema kwa filamu hii, lakini mashabiki wanapaswa kusubiri hadi Mei tutakapoiachia rasmi," alisema Lamata.
Filamu hiyo inayoakisi maisha baada ya Kanumba kufariki, imewashirikisha wasanii kadhaa wakiwamo chipukizi waliotamba katika 'This is It' na 'Uncle JJ', Khanifa Daud 'Jennifer' na Othman Njaidi 'Patrick'.
Wengine walioigiza filamu hiyo ni Philemon Lutwazi 'Uncle D', Irene Paul, Patcho Mwamba, Mainda Suka, Shamsa Ford, Jacklyne Wolper na Stanley Msungu.

No comments :

Post a Comment