Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Monday, April 1, 2013

TASWA FC, TASWA QUEENS ZANG'ARA BONANZA LA PASAKA DAR






Mwandishi wetu
TIMU ya soka na Netiboli za Waandishi wa Habari za michezo nchini, Taswa FC na Taswa Queens zimemaliza maadhimisho ya sikukuu ya Pasaka kwa kishindo baada ya kuwatambia wageni wao, timu ya Kiliflora ya Arusha.
Katika mchezo wa soka, uliochezwa kwenye uwanja wa TCC Chan'ombe Taswa FC iliibuka na ushindi wa mabao 4-1 wakati katika mchezo wa netiboli uliochezwa pia kwenye uwanja huo huo, Taswa Queens iliyokuwa inacheza kwa mara ya kwanza baada ya miaka 18 iliibuka na ushindi wa mabao 28-8.
Taswa FC ilianza mechi hiyo kwa kasi na kufana mashambulizi ya mengi hata hivyo, washambuliaji wake, Julius Kihampa na Shafii Dauda walikosa mabao mengi ya wazi.
Katika mechi hiyo, kipa wa Taswa FC, Said Seif alikuwa ‘likizo’ kufuatia safu ya ulinzi chini ya Muhidin Sufiani, Fred Mweta, Sweetbert Lukonge, Fred “Chuji” Mbembela kuwa imara muda wote huku safu ya kiungo ilichezwa na Ali Mkongwe, Wilbert Molandi, Majuto Omary na Evarist Hagila kutotoa mwanya kwa Kiliflora kupenya na kupeleka mashambulizi.
Baada ya kosa kosa hizo, Taswa FC iliandika bao lake la kwanza katika dakika ya 24 kufuatia gonga safi za Majuto “Ronaldo De Lima” Omary na Ali Mkongwe kabla ya mpira kumfikia Hagila na kuuweka kimiani.
Bao hilo lilionekana kuwachanganya Kiliflora na kujikuta wakipachikwa bao la pili kupitia kwa Dauda baada ya pasi nzuri ya Wilbert Molandi  aliyecheza vyema na Sweetbert Lukonge na kufanya timu hiyo kuongoza kwa mabao 2-0 mpaka mapumziko.
Taswa Fc ilifunga bao la tatu kupitia kwa Hagila baada ya pasi kupata pasi safi ya Fred Mbembela ‘Chuji’ na baadaye Dauda kufunga la bao la nne kufuatia ngazi nzuri ya Majuto.
Katika netiboli, ikiongozwa na Imani Makongoro aliyecheza nafasi ya (GS), Taswa Queens iliifunika kabisa Kiliflora Queens baada ya kuongoza kwa 16-3 hadi Mapumziko.
Wachezaji wengine wa Taswa Queens waliocheza mechi hiyo mbali ya Imani ni Oliver (mwananchi), Sada Ayoub,  Johari William, Elizabeth Mbassa, Shaarifa Mustapha wote wakitokea Business Times. Timu hiyo ilikuwa chini ya makocha, Amina Mussa (BTL) na Zainab Ramadhan (TBC).
 Mwenyekiti wa TASWA, Juma Pinto akikagua timu ya Netiboli ya Kiliflora ya Arusha, kabla ya kuanza kwa mchezo huo jana.
Mwenyekiti wa TASWA, Juma Pinto, akikagua timu ya Netiboli ya TASWA Queens, kabla ya kuanza kwa mchezo huo jana.
Picha ya juu ni TASWA Fc katika picha ya pamoja na ya chini ya 
Kiliflora ya Arusha, kabla ya kuanza kwa mchezo huo jana. Picha Zote na Nasma Mafoto 
www.sufianimafoto.com

No comments :

Post a Comment