Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Sunday, April 14, 2013

Mtandao wa Wasanii Tanzania (SHIWATA) kuwaonesha wasanii Aprili 24. Star Light Hotel bule


Mtandao wa Wasanii Tanzania (SHIWATA)

 

Peter Mwenda

                                 PRESS RELEASE

 SHIWATA imeandaa maonesho maalum kila mwezi ili kutoa nafasi kwa wasanii wa fani ya mbalimbali pamoja na wanamichezo kuonesha vipaji vyao.

 Wasanii wengi chipukizi wanakosa mahali pa kuonesha kazi zao, mara nyingi kazi za wasanii wakubwa ndizo ambazo hurushwa katika redio na luninga (TV).

 SHIWATA imeamua kuandaa maonesho haya kwa malengo makuu yafuatayo

(1)   Kukuza vipaji

(2)   Kuwapatia soko (underground) mahali ambapo wanaweza kuonesha vipaji vyao na kuwashawishi mapromota mbalimbali kuwaajiri.

(3)   Kuelimisha jamii kuhusu matatizo mbalimbali kama maadili na magonjwa kama UKIMWI,malaria.

(4)   Kuimarisha umoja kati ya wasanii na wanamichezo

 SHIWATA inawataarifu viongozi mbalimbali na makundi ya sanaa na Michezo pamoja na wasanii binafsi kutakua na mkutano Siku ya Jumatano Aprili 17 mwaka huu saa 8 mchana katika ukumbi wa Splendid,Bungoni Ilala kupanga ratiba na kupata taarifa zaidi.

Onyesho la Kwanza litaoneshwa katika ukumbi wa Star Light Hotel, Mnazi Mmoja Dar es Salaam siku ya Jumamosi Aprili 24.

 Michezo itakayoneshwa ni pamoja na maigizo, sarakasi, ngoma, kwaya, karate, Taekwondo, Taarab, Dansi, Bongo Flava, Mavazi, Gospal na Kasida, mada kuu katika maonesho hayo ni Amani na Utulivu.

 Hii ni nafasi ya pekee kwa wasanii chipukizi (underground) kuonesha vipaji vyao.Watengenezaji wa filamu, mapromota, wamiliki wa bendi, MaDj na wanunuzi wa mbalimbali wa kazi za sanaa wanaalikwa ili waweze kuona vipaji na kununua kazi za wasanii hao chipukizi.

 Wanafunzi wenye vipaji kutoka shule za msingi, Sekondari na vyuo mbalimbali wanaalikwa kuja kuonesha vipaji vyao.

 Mipango iliyofanywa ili maonesho haya yarushwe live kituo kimojawapo cha televisheni.

 Kutokuwa na chakula kwa wasanii na zawadi mbalimbali zinazotolewa kwa wasanii watakaofanya vizuri katika kila onesho.

 Hii itakuwa nafasi nzuri kwa wapenzi wa burudani ya sanaa kwani kwa muda mrefu walikuwa hawajui wapi wanaweza kupata burudani kama hiyo kiingilio kitakuwa bure.

 

Wote mnakaribishwa

 

Peter Mwenda 0715/0752- 222677

Ofisa Habari wa SHIWATA

No comments :

Post a Comment