Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Tuesday, April 2, 2013

Onesmo ngwi awasili Jiji la Gaborone





Rais wa IBF katika bara la Afrika, Ghuba ya Uajemi na Mashariki ya Kati, Mtanzania Onesmo Ngowi amewasili katika jiji la Gaborone, Botswana kupromoti ubingwa wa IBF wa Kimataifa katika uzito wa Bantam.  
Bondia wa Botswana Lesley Sekotswe na bondia mwenzake kutoka nchini Namibia Immanuel “Prince” Naidjala walitoka sare wakati wakishindania ubingwa huo katika pambano lililofanyika katika jiji la Windhoek, Namibia tarehe 20 Mei  mwaka huu.  
Ujio wa Rais Ngowi ulikuwa unangojewa na wadau wengi wa ngumi katika nchi hii tangu aitembelee Botswana mwaka 2002 wakati wa mpambano kati ya bondia wa Botswana Thuso Kubamang na Peter Malinga kutoka nchini Afrika ya Kusini.  
Rais Ngowi atakutana na viongozi wa serikali ya Botswana pamoja na wadau mbalimbali wa ngumi na safari yake itaanzia jiji kuu la Gaborone mpaka jiji la pili kwa ukubwa la Francistown ambako wadau wengi wa ngumi wanamsubiri kwa hamu.  
Nchi ya Botswana ni nchi yenye msingi mzuri sana wa ngumi za ridhaa lakini tatizo kubwa limekuwa ni namna ya kuwaendelza wanapofikia kikomo kwenye ridhaa. Kikao cha Ngowi na viongozi wa serikali wa Botswana kitaweka msingi mzuri wa namna ya kuwaendeleza mabondia wa Botswana. 
Botswana ni nchi inayopakana na Namibia kwa hiyo mpambano wa Sekotswe na Naidjala unategemewa kuwa na wapenzi wengi wa ngumi kutoka katika nchi hizi mbili.

No comments :

Post a Comment