Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Monday, January 14, 2013

CHANETA KUADHIBU MIKOA AMBAYO HAIJAFANYA UCHAGUZI



Chama cha netiboli nchini (CHANETA) kimesema kitatoa adhabu kwa viongozi wa mikoa ambayo haijaitisha uchaguzi wa viongozi bila ya kutoa sababu za msingi.

Kaimu Katibu Mkuu wa CHANETA, Rose Mkisi amesema mikoa hiyo tayari viongozi wake wamemaliza muda wao lakini wanashindwa kuitisha uchaguzi wa viongozi.

Mkisi aliitaja mikoa hiyo ambayo iko hatarini kupewa adhabu na CHANETA ni pamoja na Tanga, Manyara, Arusha,Kilimanjaro Mara, na Rukwa.

Mikoa mingine ambayo bado haijaitisha chaguzi zake ni pamoja na Dodoma, Tabora, Shinyanga, Iringa,Kagera, na Kigoma.

 "Tunaomba mikoa hiyo ifanye chaguzi ili kufanikisha CHANETA kuitisha uchaguzi mkuu, bila ya kufanya hivyo itapewa adhabu," aliongeza  Mkisi.

 Mkisi aliongeza  mikoa hiyo ndio chanzo kikubwa cha CHANETA kuchelewa kuitisha uchaguzi mkuu kwa ajili ya kupata viongozi wapya watakaokiongoza chama hicho kwa muda wa miaka minne.

Mkisi aliitaja mikoa ambayo tayari imefanya chaguzi zake ni kuwa ni pamoja na Dar es Salaam, Mwanza, Lindi, Mtwara,Morogoro, Ruvuma, Mbeya, na Singida.

Alisema wakitekeleza zoezi hilo mapema itakuwa rahisi kwa CHANETA kuanza harakati za uchaguzi mkuu wa kuwapata viongozi wapya wa chama hicho.

Wakati huo huo, Mkisi aliwataka wachezaji wa timu ya taifa ya netiboli kujitokeza mazoezini kwa ajili ya kujiandaa na mashindano ya kimataifa yaliyopo kwenye kalenda ya mwaka.

 mazoezi hayo kwa sasa yatakuwa yanakwenda na kurudi nyumbani chini ya makocha Mary Protasi na Mary Waya kwa ajili ya kuiandaa timu hiyo na mashindano ya kimataifa yaliyopo kwenye kalenda ya mwaka. Aliongeza  wachezaji wote wanatakiwa kuhudhuria mazoezi hayo ili iwe rahisi kwa kocha kuweza kuchagua kikosi cha kwanza cha timu hiyo kitakachoiwakilisha nchi kwenye mashindano ya kimataifa.

No comments :

Post a Comment