Waziri Mkuu
 Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward Lowassa akiongozana na
 Katibu Mkuu Mstaafu wa uliokuwa Umoja wa Nchi huru za Kiafrika 
(OAU),Dr. Salim Ahmed Salim ambaye ni Makamu Mwenyekiti wa Tume ya 
Katiba, mara baada ya Mh. Lowassa kutoa maonai yake mbele ya tume hiyo.
Waziri Mkuu
 Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward Lowassa akiwa katika 
picha ya pamoja na baadhi ya wajumbe wa kukusanya Maoni ya Katiba 
mpya,mara baada ya kutoa maoni yake.
Waziri Mkuu
 Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward Lowassa akipongezwa na
 Mjumbe wa Tume ya Kukusanya Maoni ya Katiba mpya,Dk. Senkondo Mvungi 
mara baada ya kutoa Maoni yake.
YAFUATAYO NI SEHEMU YA MAONI ALIYOYATOA MH. EDWARD LOWASAA:
Kwanza 
ningependa kukupongeza wewe mwenyekiti Mh Jaji Warioba pamoja na tume 
nzima kwa imani kubwa ambayo Rais ameionesha kwenu, ni kwa kuwapa jukumu
 hilo zito na muhimu kwa nchi yetu.
Wananchi 
pia wamekuwa na imani kubwa na wamejenga matumaini ya kila kitu kwa tume
 hii. Kutokana na hilo wamekuwa wakitoa maoni ambayo mengine hayahusiani
 na katiba, yaani siyo ya kikatiba.Pengine na mimi nitakuwa miongoni 
mwao, kwa hiyo naomba radhi mapema, iwapo maoni yangu haya mengine , 
yataonekana si ya kikatiba.
Katiba yetu
 ya sasa ni nzuri, imetuongoza katika umoja na mshikamano wa kitaifa kwa
 muda wote huo.Lakini, kutokana na hali ya dunia ya sasa, ni vyema 
kuwepo na katiba mpya ili kuendana na hali halisi.
Kuna mambo manne ambayo kwa imani na mtizamo wangu ningependa yawemo katika katiba yetu ijayo.
1.ELIMU BURE
Moja ya 
haki za mtoto ni kupata elimu. Ningependa suala la elimu bure ya 
sekondari liwemo kwenye katiba yetu. Katiba itamke wazi kuwa elimu ya 
sekondari ni bure.Nchi yetu bado ina idadi kubwa ya watu wake ambao ni 
masikini.
Uwezo wao 
wa kipato ni mdogo.Naamini kabisa hili linawezekana na serikali inaweza 
kugharimia elimu ya sekondari ikawa bure. Hii itatoa nafasi ya kujenga 
taifa lijalo lenye idadi kubwa ya vijana watakaokuwa wamepata elimu ya 
sekondari.Wabunge wenzangu bila shaka wanalijua hili.
Ukweli katika majimbo yetu wazazi wamekuwa wakishindwa kulipia karo ya shule kwa 
 watoto wao. Wabunge tumekuwa tukibeba mzigo huo japo kidogo. Kwa hiyo, 
kifungu cha ELIMU BURE KWA SEKONDARI, kiwepo kwenye katiba.
2.ADHABU YA KIFO-DEATH PENALT
Katiba ya 
sasa haisemi wazi kuhusu adhabu ya kifo.Inazungumzia tu haki ya 
uhai.Ibara ya 14 ya katiba hii ya jamuhuri ya muungano wa tanzania ya 
mwaka 1977 inatamka kiujumla tu kuwa KILA MTU ANA HAKI YA KUISHI NA UHAI
 WAKE KULINDWA.
Lakini , 
haki hiyo inanyang'anywa na kifungu nambari 196 cha sheria ya kanuni za 
adhabu sura ya 16(penal code ,cap 16), kinachotamka kuwa adhabu ya 
kifo(death penalty or capital punishment) kwa kosa la mauaji ya 
kukusudia.
Adhabu hiyo
 hiyo pia utolewa kwa kosa la uhaini.Sasa mapendekezo yangu mimi ni 
kwamba kuwe na ibara katika katiba mpya inayotamka wazi kuwa HAKUTAKUWA 
NA ADHABU YA KIFO HAPA NCHINI HATA KWA KOSA LA KUKUSUDIA AU UHAINI.
3.MATUMIZI YA FEDHA KATIKA UCHAGUZI
Katika 
sehemu nyingi hapa nchini mwananchi kama hana fedha hawezi kugombea 
nafasi mbalimbali za uongozi.Katiba mpya iwe na ibara inayofafanua ni 
kiasi gani cha fedha ambacho mgombea anaruhusiwa kutumia katika 
kampeni.Iainishe ni matumizi gani ya lazima ambayo mgombea hawezi 
kukwepa kutumia fedha katika kampeni zake, mfano kuwakusanya wapiga kura
 kwenda kupiga kura gharama hizo nani azibebe.
Katiba 
ifafanue rushwa ni nini kwenye chaguzi hizi.Au tuwe na mfumo wa 
PROPORTIONAL REPRESENTATION ,vyama viwe ndiyo vinaingia kwenye chaguzi 
kuwania majimbo na siyo wanachama,huko kila mtu atakuwa anapigania chama
 chake kupata kura nyingi ili wapate viti vingi zaidi, pengine hii 
itasaidia kuondoa kikwazo cha mtu kuwa na uwezo wa kifedha ndiyo aweze 
kuwania uongozi.
4.ARDHI
Kwa 
mwanadamu, kunyang'anywa haki ya kutumia ardhi ya nchi aliyozaliwa ni 
sawa na kunyanng'anywa haki ya uraia wake. Katiba hii ya sasa inawapa 
nguvu wakulima katika suala la ardhi, na kuwasahau wafugaji.
Wafugaji 
wamekuwa wakimbizi katika nchi yao, wamekuwa wakitangatanga kutafuta 
malisho ya mifugo yao, ile ardhi waliyokuwa wanaimiliki wakiondoka 
kutafuta malisho huku nyuma imekuwa ikimilikishwa watu wengine, wakulima
 au wawekezaji, hili kwakweli si jambo jema .
Tumeshuhudia
 migogoro ya ardhi kati ya wakulima na wafugaji.Kwa hiyo, mimi 
ningependa katiba hii mpya impe mfugaji haki katika suala la ardhi 
kama.Ardhi ya wafugaji ilindwe, ifafanuliwe kikatiba haki yao hiyo. Kuwe
 na hali ya 50,50 situation kati ya mfugaji na mkulima katika suala zima
 la umiliki wa ardhi,kikatiba!
No comments :
Post a Comment