Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Thursday, January 17, 2013

FILAMU YA REAL PROMISE KUTOKA HIVI KARIBUNI




Na Elizabeth John
KAMPUNI ya Faisal Production ikiwa miongoni mwa taasisi chache zenye lengo maalum la kuhakikisha fani ya filamu inastawi na kupata maendeleo nchini, imeandaa kazi mpya inayokwenda kwa jina la ‘Real Promise’.

Katika filamu hiyo ambayo tayari imeanza kuwa gumzo la jiji, waigizaji nyota kama Mohammed Mwikongi ‘Frank’, Rose Ndauka, Bambucha na Rania wameshiriki na kufanya makubwa ambayo yatamfanya mtazamaji kutopata muda wa kufanya shughuli nyingine.

Kwa mujibu wa msemaji wa kampuni hiyo, Mohammed Njiriku, filamu hiyo kwa sasa iko katika hatua ya uhariri, akisisitiza kutoa tungo bora kabisa sambamba na kuchezwa vizuri na wahusika.

Real Promise inazungumzia mikasa ya mapenzi na hatua mbalimbali za kukabiliana nayo ikizingatiwa kuwa mapenzi ni sehemu kubwa ya maisha ya kila siku ya binadamu.

Rose, ambaye ameng’ara katika filamu nyingi hapa nchini, amefanya makubwa katika kazi hiyo inayotarajiwa kutoka wakati wowote mwezi huu.

No comments :

Post a Comment