Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Monday, January 28, 2013

MASHAIRI YAMUUMIZA KICHWA PINGU




Na Elizabeth John
MSANII wa muziki wa kizazi kipya nchini, Ramadhani Kalesela ‘Pingu’ amesema kuwa anafanya uchaguzi wa nyimbo alizonazo ili kuachia mojawapo ambayo itakonga na kuteka soko la muziki nchini.

Akizungumza na Habari Mseto jijini Dar es Salaam, Pingu alisema anapata wakati mgumu kuchagua wimbo wa kuachia kutokana na kila wimbo kuwa katika kiwango cha juu.

“Nyimbo zangu zote ni nzuri kitu ambacho kinanipa wakati mgumu kuamua ni ngoma gani niachie lakini wakati wowote kuanzia sasa nitaachia baada ya kushauriana na wadau wangu,” alisema Pingu.

Msanii huyo alipata umaarufu kupitia nyimbo mbalimbali akishirikiana na Deso ambao walitoa albamu kadhaa ikiwemo inayoitwa ‘Eeh Mola’ iliyokuwa na nyimbo kama Tutasema, Hamisi, Chanzo Cha Ukoloni, Joanitha na nyinginezo.

Pia siku chache zilizopita msanii huyo aliachia ngoma yake ambayo haikufanya vizuri iliyoitwa ‘Zarumenda’ na sasa anajipanga upya kuhakikisha na anarudi tena katika tasnia hiyo akiwa pamoja na Deso.

No comments :

Post a Comment