Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Thursday, January 17, 2013

PNC KUFANYA MAGEUZI KATIKA MUZIKI WA KIZAZI KIPYA




Na Elizabeth John
BAADA ya kimya cha muda mrefu, msanii wa muziki kizazi kipya, Pancras Ndaki Charles ‘PNC’, ameibuka na kusema amerudi kufanya mageuzi makubwa katika muziki huo na kumtaka msanii mwenzake Naseeb Abdul ‘Diamond Platinum’ ajiandae kuvaa vumbi.

Akizungumza na Habari Mseto Blog, PNC, amesema kuwa ukimya wake haukuwa bure bali alikuwa anajipanga vema na ujio wake mpya umekuja huku Diamond akioneka kuliteka anga la muziki huo na kumtambia kuwa muda si mrefu atamfunika.

“Nilikaa kimya muda mrefu baada ya kutamba na ngoma yangu ya ‘Mbona’ niliyomshirikisha Mr Blue, na kipindi chote nilikuwa najaribu kuangalia jinsi nitakavyoliteka anga la muziki huu, na ujio wangu mpya umekuja wakati Diamond akiwa safi, hivyo asubiri kuvaa vumbi kwani nitampoteza vibaya,” alisema PNC.

PNC anayesimamiwa na meneja wake makini, Ostaz Juma, chini ya lebo ya Mtanashati Entertainment, alisema hivi karibuni anatarajia kuachia ngoma yake mpya ambayo hajataka kuitaja jina kutokana na maharamia waliopo katika tasnia hiyo.

Mmsanii huyo ambaye ndiye kiongonzi wa kundi la Mtanashati Entertainment, anawaomba wadau na mashabiki wa muziki huo kukaa mkao wa kula kwaajili ya kuzipokea kazi zao zinazokuja.

No comments :

Post a Comment