Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Thursday, January 17, 2013

WASHINDI WA PROMOSHENI YA WESTERN UNION WAPATIKANA



 Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Posta Tanzania (TPB), Sabasaba Moshingi, akisoma namba ya mshindi wa zawadi ya sh. miloni mbili ya promosheni ya mwisho ya huduma ya Western Union, itolewayo na benki hiyo, wakati wa kuchezeshwa droo hiyo jijini Dar es Salaam leo. (Picha na Habari Mseto Blog)
 Mkurugenzi Mkuu wa Benki hiyo, Sabasaba Moshingi  akifafanua jambo wakati wa kuchezesha droo hiyo.
 Mkurugenzi Mkuu wa Benki hiyo, Sabasaba Moshingi (katikati) akimsikiliza kwa makini Meneja wa benki hiyo tawi la Kariakoo, Maduhu Bulebi Makoye wakati wa kuchezesha droo hiyo. Kushoto ni Meneja Mkuu Mauzo na Huduma kwa Wateja, Grace Nkuzi. 

Na Mwandishi Wetu

BENKI ya Posta Tanzania (TPB), imetangaza washindi watatu wa promosheni ya Shindano la  kutumia huduma ya Weastern Union, ambalo ni la pili, baada ya lile la mwaka jana.

Akizungumza leo jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi Mkuu wa Benki hiyo, Sabasaba Moshingi amesema kuwa washindi hao watatu wamepatikana baada ya droo iliyochezeshwa mbele ya waandishi wa habari.

"Washindi hao wametoka katika matawi mbalimbali ya Benki ya Posta nchini ambapo zawadi ya kwanza na ya pili zimebaki jijini Dar es Salaam na ile ya tatu kwenda mkoani Arusha".

Moshingi aliwataja washindi hao kuwa ni pamoja na James Mkondya aliyejinyakulia sh milioni mbili, Ensel Issa, sh milioni mojawote hao wakazi wa jijini na Kaeni Kapangi aliyejinyakulia sh 700,000 mkazi wa Arusha.  

Aidha,  washindi  wengine kumi wamejipatia zawadi ya sh 100,000 kila mmoja.

Moshingi alitoa wito kwa Watanzania kujiunga na huduma za Benki hiyo kwani zimboreshwa na kuwafanya wateja wake kwenda na wakati katika shughuli zao zakujiletea maendeleo.

No comments :

Post a Comment