* Asema kuwapa uongozi Chadema ni sawa na kumkabidhi Bucha Fisi
NA BASHIR NKOROMO, GEITA
CHAMA
 Cha Mapinduzi (CCM) kimetaka Mwenyekiti wa Serikali ya Kijiji cha 
Katoro Mazemule  na wenzake wanaodaiwa kuhusika na wizi wa sh. milioni 
16.5 za Halmashauri ya kijiji hicho wafikishwe mahakamani haraka.
Akizungumza
 kwenye mkutano wa hadhara leo, katika mji mdogo wa Katoro, mkoani 
Geita, Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye alisema, ni lazima 
wahusika wote wa wizi wa fedha hizo wafikishwe mahakamani kwa kuwa ni 
jasho la wananchi.
Fedha
 hizo zinadaiwa kuliwa na Mwenyekiti huyo kwa tiketi ya Chadema, katika 
kipindi cha mwaka 2010 na 2011 hali ambayo imezusha tafrani miongoni mwa
 wananchi na uongozi wa Halmashauri ya Kijiji hicho hadi sasa.
Nape
 alisema, ni lazima Mwenyekiti huyo na waliohusika wote wafikishwe 
mahakamani kwa kuwa kamati iliyoundwa kuchunguza upotevu wa fedha hizo 
ilishamaliza kazi yake na ripoti kukabidhiwa kwa mamlaka zinazohusika.
"Kamati
 ya kuchunguza wizi wa fedha hizi ambazo ni mali ya wananchi ilishafanya
 kazi yake na kukabidhi ripoti kwa mamlaka zinazohusika, sasa 
kinachosubiriwa ni nini wahusika hawa kupelekwa mahakamani?", Nape 
alihoji na kuongeza;
"Sasa
 CCM kwa kuwa ndicho chama tawala, tunaagiza hatua za kuwapeleka 
mahakamani wahusika wote zichukuliwe haraka ili haki itendeke".
Nape
 alisema, kutotokea kwa wizi wa fedha hizo chini ya uongozi wa 
Halmashauri ya Kijiji hicho ambao upo chini ya chama hicho, ni dalili 
kwamba kujidai kwao kuwa wasafi na wapigania haki za wanyonge ni sawa na
 kilio cha mamba.
"
 Kila mara tumekuwa tukiwaambia acheni kuhadaiwa na Chadema, hawa siyo 
chama cha siasa ni kundi la wajanja fulani, sasa Wana Katoro mmejionea 
wenyewe, mmewajaribu mkawapa halmashauri yenu, fedha wamezitafuna sasa 
mnahangaika", alisema na kuongeza;
"Kwa
 kuwa mmepata funzo hili, bila shaka hamtaruidia tena, kwani 
mmeshafahamu kwamba kuikabidhi uongozi Chadema ni sawa na kumkabidhi 
fisi bucha".
Mapema,
 Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Geita, Joseph Msukuma, alisema kwenye mkutano
 huo kwamba, kama hatua za kuwafikisha mahakamani wahusika 
hazitachukuliwa haraka, ataongoza wananchi wa Katoro kuandamana ili 
kuhakikisha hatua hizo zinachukuliwa.
Kabla
 ya mkutano huo, NMape alifungua shina la wajasiriamali la CCM, 
Bugayambele lenye wanachama  53 ambao hushughulika na kazi za kutengeza 
fenicha mbalimbali katika karakana yao iliyopo eneo hilo la Katoro.
Akifungua
 shina hilo, Nape aliahidi kuwapa sh. milioni moja kwa ajili ya 
kuendeleza shughuli zao, ikiwa ni pamoja na kununua vitendea kazi kama 
randa za mbao, mashine ya kuchetrza mbao na ujenzi wa banda kwa ajili ya
 shughuli hizo.
No comments :
Post a Comment