Meneja wa 
Swahili Fashion Week, Washington Benbella akizungumza na waandishi wa 
Habari wakati wa uzinduzi wa Swahili Fashion Week 2012. Kutoka kushoto 
ni Hassan Mrope, Meneja Mahusiano wa Swahili Fashion Week, Happy Shame 
Meneja Masoko EATV..JPG
DAR ES SALAAM, Tanzania
Onyesho 
kubwa la mitindo la Afrika Mashariki na kati linarajiwa kufanyika siku 
tatu mfululizo katika Hoteli ya Golden Tulip kuanzia tarehe 6, 7 na 8 
Desemba, 2012 ikiwa ni mara ya tano tangu kuanzishwa kwake.
Swahili 
Fashion Week 2012 kwa ujumla itakutanisha pamoja wadau 50 katika tasnia 
ya Mitindo kutoka nchi zinazozungumza Kiswahili na nyengine kuweza 
kuonyesha ubunifu wao na kutoa mustakabali wa mwenendo wa tasnia ya 
mitindo katika ukanda huu.
“Mwaka 
tumekuwa kwa kiasi kikubwa, wabunifu 23 kutoka Tanzania wataweza 
kuonyesha ubunifu wao na wengine waliobaki ni kutoka nje ya Tanzania, 
ambao wote wataonyesha ubunifu wao katika jukwaa moja ukiachilia 
wabunifu 16 walionyesha ubunifu wao katika maonyesha ya Swahili Fashion 
Week yaliyofanyika Nairobi, Kenya, Oktoba 6, 2012” Alisema Meneja wa 
Swahili Fashion Week, Washington Benbella
Katika 
kuongeza maonyesho ya mitindo, mwaka huu Swahili Fashion Week shopping 
Festival ambayo ilianza 2010 itakuwepo tena kwa mara nyengine ambapo 
itashirikisha zaidi ya waonyeshaji 30 katika sehemu moja ikiwa ni kwa 
ajili ya kuonyesha na kuuza bidhaa za ubunifu hivyo kuifanya kuwa msimu 
mkubwa manunuzi ya kazi za ubunifu wa mitindo hapa Tanzania.
Kama 
ilivyo ada, Swahili Fashion Week inatoa nafasi kwa kuendeleza vipaji, 
ambapo tarehe 24 Novemba, 2012 kutakuwa na mchujo wa wazi kwa 
wanamitindo wapya na wanaochipukia kwa jinsia zote, na mnamo tarehe 7 
Desemba, 2012 kutakuwa na warsha kwa ajili ya wabunifu wote Tanzania 
chini wadhamini wakuu wa warsha hiyo USAID Compete ambayo itafanyika 
katika Hotel ya Golden Tulip” Aliongeza Benbella
Mashindano
 tofauti yamepangwa kufanyika wakati wa Swahili Fashion Week, ikiwemo 
Shindano la kumtafuta Mbunifu Bora anaechipukia na Mbunifu Bora wa 
kubuni Fulana. Sio tu inatoa changamoto na ari ya ushindani katika 
tasnia ya ubunifu nchini Tanzania, bali pia inaweka msingi imara kwa 
wabunifu wa baadae.
“Sherehe 
maalum za kufungua Swahili Fashion Week zinarajiwa kufanyika siku ya 
Jumapili tarehe 25 Novemba, 2012, Thai Village kuanzia saa 9 usiku. 
Sherehe hizo pia zitafuatiwa na kutangazwa kwa majina ya waliochaguliwa 
kushindania tuzo mbalimbali zilizowekwa katika vipengele 16, tuzo hizi 
ni za kwanza na ndio pekee katika ukanda huu. Tiketi za sherehe za 
uzinduzi wa Swahili Fashion Week 2012 zinapatikana sehemu zifuatazo, 
Thai Vilage, Mgahawa wa Epidor uliopo Masaki, na Tanzania Mitindo House”
 Alisema Meneja Uhusiano, Hassan Mrope
“Tukiwa 
na mipango yenye ndoto za kutangaza biashara ya mitindo katika ukanda wa
 Afrika mashariki na kati, ninapenda kuchukua nafasi hii kuwashukuru 
washirika wetu pamoja na  wadhamini wetu ambao karibia ya wote wamekuwa 
wakitusaidia kutokea maonyesha yaliyopita mpaka sasa. Pia tuwashukuru 
sana watu wote wanaosaidia tasnia ya mitindo hapa Tanzania kwa si tu 
kuhudhuria matamasha na maonyesho kama haya bali pia kwa kununua bidhaa 
zinazotengenezwa hapa nchini kwani hii inatangaza kinachotengenezwa 
Africa “Made in Africa”. Alimalizia Benbella

No comments :
Post a Comment