Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Friday, November 30, 2012

MKUTANO MKUU WA NAMANGA SPORTS CLUB KUFANYIKA DESEMBA 09 NDEGE BEACH



Mwenyekiti wa Namanga Sports Club, David Mwaka akiongoza kikao cha maandalizi ya Mkutano Mkuu Maalum wa Klabu, kilichofanyika Leecar's Pub Namanga jijini Dar es Salaam. PICHA/JOHN BADI
xxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx

- KONYAGI yaupiga 'Jeki'

Na John Badi
 
Mkutano Mkuu Maalum wa Klabu ya Namanga Sports unatarajiwa kufanyika Desemba 09, mwaka huu katika Ukumbi wa Ndege Beach uliopo katika eneo la Mbweni nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam.

Akizungumza wakati wa kikao cha maandalizi, Mwenyekiti wa Namanga Sports Club, Bw. David Mwaka alisema tayari makampuni kadhaa yameshajitokeza kudhamini mkutano huo.

Bw. Mwaka aliyataja makampuni hayo kuwa ni pamoja na Tanzania Distilleries Ltd watengenezaji wa kinywaji maarufu cha Konyagi, Mike Commercial, Esoshi General Trading Co. Ltd na Mele DJ Co. Ltd ya Dodoma.

"Tunawashukuru sana wadhamini ambao tayari wamekwisha onyesha moyo wa kutusaidia, lakini pia tunawaomba wadhamini wengine wajitokeze zaidi ili tuweze kufanikisha mkutano wetu", alisema Bw. Mwaka.

Aidha Bw. Mwaka alitoa wito kwa wanachama wa klabu hiyo ambao bado hawajatoa michango yao ya 20,000/- kuiwasilisha mara moja kwa watu waliopewa majukumu ya kukusanya ambao ni John Gako, Bebee Mangi na Chale JJ.

No comments :

Post a Comment