Meneja Mkuu wa Multichoice Tanzania 
Bw. Peter Fauel, akitangaza Punguzo la Asilimia Kumi ya Malipo ya mwezi 
kwa wateja wa Televisheni kwa Vipindi vya DStv likaloanza hapo kesho, 
ambapo amesema punguzo hilo litawawezesha wateja wao kulipia huduma za 
Matangazo ya Televisheni ya kituo hicho kwa gharama nafuu. Pia amesema 
Offer hiyo ya Punguzo la bei ni hatua ya Kampuni hiyo kurudisha fadhila 
kwa wateja wake kuelekea katika kipindi cha maadhimisho ya sikukuu za 
mwisho wa mwaka. Kulia ni Meneja Uhusiano wa Kampuni ya Multichoice 
Barbara Kambogi na Kushoto ni Meneja Masoko wa Kampuni hiyo Bi. Furaha 
Samalu.
Meneja Masoko wa Multichoice wa 
Kampuni hiyo Bi. Furaha Samalu akitoa ufafanuzi kuwa katika kipindi hiki
 cha kuelekea matumizi ya mfumo wa Digitali DStv kwa kuwajali wateja 
wake imepunguza gharama za kuunganishwa ambapo sasa ni kwa shilingi za 
Kitanzania 169,000 unaweza kusheherekea msimu wa sikukuu na DStv.
Meneja Uhusiano wa Kampuni ya Multchoice Barbara
 Kambogi (wa pili kushoto) akiwahakikishia wateja wa DStv kuwa sasa 
kampuni hiyo imezidi kuboresha huduma zenye viwango vya hali ya juu na 
kuwataka wazazi kutumia fursa hii ya punguzo la bei ya kuunganishwa ili 
watoto wao waweze kushuhudia vipindi mbali mbali vya kuelimisha na 
kuburudisha ikiwemo filamu kali, katuni maridadi, michezo mbalimbali 
katika kipindi hiki cha likizo kwa watoto wao na kuwa huu ndio sasa muda
 muafaka kwa kujipatia DStv.
 Meneja 
Mauzo wa DStv Tanzania Bw. Salum Salum akifafanua kuwa Multichoice 
imepanua wigo wa kutoa huduma kwa wateja ambapo sasa wanamawakala 200 
nchini na kuwataka  wanapokwenda kulipia Ving'amuzi vyao ni lazima 
wahakikishe vimewashwa ili kurahisisha kufanyika kwa huduma hiyo pia 
amesema wateja wa DStv wanaweza kufanya malipo ya huduma hiyo kupitia 
simu za mkononi na ukizingatia kampuni hiyo imeongeza maeneo ya kutoa 
huduma ikiwemo Uchumi Super Market, Kariakoo na Mlimani City kwa wakazi 
wa Dar es Salaam.
No comments :
Post a Comment