Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Wednesday, November 28, 2012

KUMUONA JB MPIANA 100,000





 JB Mpiana akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam kuhusu shoo yake itakayofanyika Leaders Club Novemba 30.
Mtangaji wa Kituo cha Televisheni cha Channel Ten, Said Kilumbanga (kulia) akiwa amepozi na wanenguaji wa  mwanamuziki kutoka Congo, JB Mpiana
DAR ES SALAAM, Tanzania
MSANII nguli wa muziki wa dansi Afrika, JB Mpiana amewataka Watanzania kujitokeza kwa wingi na kushuhudia shoo yake itakayopigwa kwenye viwanja vya Leaders Club jijini Dar es Salaam Ijumaa hii, ambapo kiingilio kwa VIP A itakuwa sh 100,000 na kawaida sh 25,000.

Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, JB Mpiana alisema, anajikubali na kuithamini kazi yake ambayo anaifanya na kuahidi kuwapa raha wapenzi na wadau mbalimbali wa muziki hapa nchini ambao watajitokeza siku hiyo.

“Kwanza nimefurahia sana mapokezi ya jana, hivyo basi nitawapa raha siku hiyo na pia nawapongeza waandaaji kwa kuona umuhimu na kuniteua mimi kufanya nao kazi siku hiyo, nimekuja na kikosi changu kamili cha watu 25, hivyo basi nina imani siku hiyo itakuwa raha sana,” alisema Mpiana.

Mpiana aliwataka wanamuziki wa hapa nchini, kujituma na kufanya kazi zao kwa ufanisi zaidi na kuziheshimu pia, ili waweze kufikia mafanikio ambayo wamejipangia kuyafikia, kwa kuwa hata yeye alianzia huko na ndio sababu amefikia hapa alipo.

Naye Mkurugenzi wa QS J Mhonda Entertainment, Joseph Mhonda, alisema kila kitu kimekamilika na kudai kuwa, kwa sasa wanasubiri siku ifike ili watanzania wapate raha na kile ambacho wamekitarajia.
Mhonda alisema, viingilio siku hiyo itakuwa sh 25,000 kwa atakayenunua tiketi mapema, huku 30,000 kwa watakaonunulia mlangoni na sh 100,000 VIP A kwa watakaonunua mapema huku kwa mlangoni ni sh 150,000.

Aliongeza kuwa, Mpiana ataanza kufanya shoo ukumbi wa Triple A, jijini Arusha na baadaye jijini Mwanza katika ukumbi wa Villa Park huku wasanii mbalimbali wakitarajiwa kutumbuiza siku hiyo ambao ni Ney Wamitego, H Baba, Mashujaa pamoja na Mb Dog.

No comments :

Post a Comment