Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Thursday, November 29, 2012

TIGO NA REACH FOR CHANGE YAKABIDHI DOLA ZA KIMAREKANI 75,000 KWA WASHINDI WATATU KILA MOJA KUPITIA SHINDANO LA WAJASIRIAMALI KUTPITIA SHINDANO LA REACH FOR CHANGE




Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Tigo, Andrew Hodgson (Kushoto) akiwa na mmoja wa wajasiliamali aliyeshinda shindano la Tigo Reach For Change, Bi. Brenda D. Shuma pamoja na Mkurugenzi wa Reach For Change Sarah Damber.
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Tigo, Andrew Hodgson (Kushoto) akiwa na washindi watatu wa shindano la Tigo Reach For Change,  Bi. Brenda D. Shuma, Nyabange Chirimi na Thadei Msumanje, kulia ni Mkurugenzi wa Reach For Change Bi.  Sarah Damber.
 Mmoja wa wajasiliamali aliyeshinda shindano la Tigo Reach For Change, Bi. Brenda D. Shuma akielezea jambo kwa waandishi wa Habari.
Meneja wa Tigo, kitengo cha huduma za Jamii Woinde Sishael akifafanua jambo mbele ya waandishi wa habari na wadau walihudhuria mkutano huo.
Wadau wakifuatilia kwa umakini.
---
Mwezi Septemba mwaka huu, Tigo kwa kushirikiana na Shirika la kujitolea la Reach For Change kwa mara ya kwanza nchini Tanzania walizindua programu iliyodhamiria kutambua na kuendeleza mawazo madhubuti ya wajasiriamali  yenye lengo la kuboresha maisha ya watoto.
Baada ya kampeni ya mwezi mmoja ya kutoa wito kwa watanzania wote wenye mawazo madhubuti kujitokeza kwa ajili ya ajili ya kuwasilisha maombi yao, tulipokea maombi 2480, ambapo waombaji 15 walifika fainali  ikifuatiwa na mchujo mkali ambao ulijumuisha wafanyakazi wa Tigo na Reach For Change pamoja na wataalamu wengine wa nje. Hawa waliendelea kuchujwa hadi tulipofanikiwa kupata washindi watatu  baada ya mawazo yao kupitishwa na jopo la majaji.
"Mpango wa kurejesha kwa Jamii sehemu ya faida yetu, ni moja ya nguzo ya kampuni yetu na tuna nia ya dhati na mpango huu wa Reach for Change, ambao ni sehemu ya mpango wetu kimataifa. Tigo Tanzania imepokea maombi yenye mvuto na ushindani wa hali ya juu. Washindi wa nafasi tatu za juu ambao wamechaguliwa leo si tu walishinda mioyo za majaji bali waliwavutia na ubunifu wa mipango yao dhubuti. Sasa waanapokea ufadhili wa $25,000 kama mshahara wa mwaka, kwa miaka mitatu mfululizo ili kuweza kuzingatia na kutimiza malengo yao," alisema Andrew Hodgson, Kaimu Mkurugenzi Mkuu Tigo.
Washindi wa shindano la wajasiriamali la Tigo Reach For change mwaka 2012 ni Brenda-Deborah Shuma, Nyabange Chirimi na Thadei Msumanje. Miradi yao watakayo ianzisha italenga katika kuwawezesha watoto wenye ulemavu na vijana wenye ujuzi wa kiufundi, kusaidia elimu ya watoto wa mitaani na kuboresha elimu kupitia Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (ICT).
'Tigo Reach for Change' imelenga katika kuainisha na kusaidia wajasiriamali kwenye miradi ya kijamii na wenye mawazo yakinifu juu ya kuboresha maisha ya watoto wa Tanzania. Washindi hawa watatu sasa wanajiunga na programu ya miaka mitatu ya kuboresha miradi yao, ambapo mawazo yao yatabadilishwa kuwa miradi endelevu. Mbali na hayo, watapata mshahara wa dola 25,000 kwa mwaka kwa miaka mitatu mfululizo pamoja na ushauri wa kitaalamu kutoka kwa wafanyakazi waandamizi wa Tigo.
Reach for Change ni Shirika la kujitolea lililoanzia Sweden ambalo lilianzishwa na Kinnevik, ambaye ndiye aliyeunda kampuni ya Millicom (shirika anzilishi la Tigo). Kampeni ya kutafuta wajasiriamali kwa mkakati wa Reach for Change kwa mara ya kwanza ulianzia huko Sweden mwaka 2010 ikifuatiwa na Russia 2011 kabla mwaka huo huo kuanzishwa barani AfriKa katika nchi ya Ghana. Hadi sasa imeweza kuboresha maisha ya watoto wapatao 140,000 nchini Ghana.
Tigo na Reach For Change imeanza rasmi utafutaji wa wajasiriamali kwenye miradi ya kijamii,  katika nchi zinazotoa huduma yake barani  Afrika, kwa kuzinduliwa kwanza Rwanda ikifuatiwa na Tanzania, halafu Ghana, Congo DRC, Senegal na mwishomi itakuwa Chad miezi michache ijayo.

No comments :

Post a Comment