| Wachezaji wa Zanzibar Heroes wakisujudu wakati wakishangilia goli lao la kwanza lililofungwa wakati wa mechi yao ya Kundi C la Kombe la Chalenji kwenye Uwanja wa Mandela, Kampala leo. | 
Nyota
 wa klabu ya Azam FC ya Dar es Salaam, Khamis Mcha 'Viali' alifunga mara
 mbili na kuifanya Zanzibar ifikishe pointi 4 baada ya mechi mbili na 
sasa ina uhakika wa kutinga hatua ya 8-Bora hata kwa nafasi ya ‘best 
looser’ kulingana na matokeo ya mechi za mwisho. 
Rwanda
 inayoshika nafasi ya pili ya msimamo wa Kundi C kwa kuwa pointi 3 na 
Malawi iliyo katika nafasi ya tatu kwa pointi 3 pia baada ya jana 
kushinda 3-2 dhidi ya Eritrea inayoburuza mkia, zinaweza kufikisha 
pointi 6 zikishinda mechi zao za mwisho Jumamosi. Hata hivyo, matokeo 
hayo hayataizuia Z’bar kutinga robo fainali kama ‘best looser’, endapo 
itapoteza mechi yake ya mwisho Jumamosi dhidi ya Malawi. 
Hali
 mbaya ya uwanja iliwagharimu pia Malawi na Eritrea, ambapo katika 
matukio mawili -- moja kwa kila timu -- mpira uliokuwa ikiserereka 
kuingia wavuni ulikwama kwenye dimbwi la maji kabla ya kuokolewa na 
mabeki wa timu hizo. 
Katika
 tukio la kwanza wakati Malawi wakiongoza kwa magoli 2-0 wangeweza 
kufunga goli la tatu baada ya mpira kumpita kipa na mchezaji mchezaji wa
 malawi kupiga shuti dogo katika lango tupu akidhani amefunga lakini 
mpira ulikwama kwenye dimbwi kabla ya beki kufika na kuokoa mpira.
Tukio
 jingine lilikuja wakati Eritrea wakiwa nyuma kwa magoli 2-1 na 
wangeweza kufanya matokeo yawe 2-2 lakini mpira uliokuwa ukienda wavuni 
ulinasa kwenye dimbwi na kuwapa nafasi Malawi kuokoa.  
Zanzibar
 ilipata goli la kuongoza katika dakika ya 9, shukrani kwa madimbwi ya 
maji yaliyouzuia mpira usimfikie kipa wa Rwanda, Jean Claude Ndoli, 
aliyekuwa katika nafasi nzuri ya kuuokoa jirani na ukingo wa boksi na 
kumpa mwanya Mcha kufunga katika nyavu tupu.
Mcha alifunga goli la pili katika dakika ya 62 kufuatia pasi ndefu kutoka kulia.
Rwanda
 walicharuka na kupata goli kupitia kwa Dady Birori aliyefunga kwa 
kichwa katika dakika ya 80 kufuatia krosi ‘matata’ ya nahodha Haruna 
Niyonzima.
Kocha
 wa Rwanda, Milutin Sredjovich ‘Micho’ alisema baada ya mechi hiyo 
kwamba hawezi kusingizia uwanja kwa kipigo chao kwa sababu hata 
wapinzani wao walicheza katika uwanja huo huo lakini alisema mazingira 
yalikuwa hayafai kuendelea kuchezewa mechi.
Michuano
 hiyo inaendelea kesho kwa mechi za Kundi A ambapo Kenya itacheza dhidi 
ya Ethiopia saa 10:00 jioni kabla ya wenyeji Uganda ambao tayari 
wametinga robo fainali watawakaribisha Sudani Kusini saa12:00 jioni.
No comments :
Post a Comment