Wanamuziki
 wa bendi ya Mashujaa, wakiongozwa na Chalz Baba (katikati) wakijifua 
wakati wa mazoezi yao ya maandalizi ya uzinduzi wa Albam yao ya pili 
inayokwenda kwa jina la Risasi Kidole, uzinduzi unaotarajia kufanyika 
kesho katika Viwanja vya Leaders Club, Kinondoni, huku ukisindikizwa na 
mwanamuziki mahiri kutoka Congo, JB Mpiana.
Kiongozi wa bendi hiyo, Chalz Baba, akiongoza mashambulizi wakati wa mazoezi hayo ya maandalizi leo.
************************
BENDI
 ya Mashujaa kesho siku ya Ijumaa itazindua albamu yake ya pili 
ijulikanayo kwa jina la Risasi Kidole pamoja na bendi maarufu ya Congo, 
Wenge BCBG iliyochini ya mwanamuziki JB Mpiana kwenye  viwanja vya Leaders club, Kinondoni.
Uzinduzi
 huo umepangwa kuanza saa 2.00 usiku na maandalizi yake yamekwisha 
kamilika kwa mujibu wa meneja wa bendi ya Mashujaa, Martin Sospeter. 
Sospeter alisema kuwa wamejiandaa vilivyo katika uzinduzi huo na lengo 
lao kubwa ni kuweka historia katika muziki wa Tanzania.
Alisema
 kuwa wamekaa kambini muda wa siki mbili na wameandaa vitu vingi vipya 
kwa ajili ya kuwapa burudani mashabiki wa muziki wa dansi nchini. 
Alisema kuwa kuna rap ya Ua Mbu na Dume la Simba kutoka kwa marapa wao, 
Saulo Ferguson na Sauti Radi.
Alifafanua
 kuwa wanamuziki wake wameadhimia ‘kufunika’ katika uzinduzi huo kwani 
anahistoria nzuri katika muziki wa Tanzania na kufanya kazi katika bendi
 nyingi.
“Tunawaomba
 watanzania waje waone nini tunakifanya mbele ya gwiji la muziki wa 
dansi Afrika, JB Mpiana, najua wao wamepania, lakini sisi tumepania 
vilivyo kusafisha nyoyo za mashabiki ambazo kwa sku nyingi hawajapata 
burudisha la mioyo zao,” alisema.
Kiongozi
 wa bendi hiyo, Charlz Baba alisema kuwa wamepania kutoa somo kwa 
wanamuziki wa dansi hapa nchini ambao wamekuwa wakisubiri waone 
watafanya nini. Alisema kuwa wameandaa nyimbo nyingi nzuri  na wamepatia kutawala soko la muziki hapa nchini.
“Njooni
 muone nini tunafanya katika muziki wa dansi, kambi yetu imekuwa nzuri 
na mafanikio makubwa, naomba mashabiki waje kutuunga mkono nasi 
tutawaunga mkono kwa kutoa burudani safi,”alisema Chalz.
Albamu
 ya Risasi Kidole ina jumla ya nyimbo sita. Nyimbo hizo ni Umeninyima, 
Tikisika, Hukumu ya Mnafiki, Ungenieleza, Kwa Mkweo na wimbo uliobebab 
jina la albamu hiyo, Risasi Kidole
No comments :
Post a Comment