Baadhi
 ya Wakazi wa Jiji la Dar wakiwa wanasubiri treni ya mwakyembe iwasili 
stesheni ikitokea ubungo maziwa tayari kwa safari ya kuwarudisha 
Majumbani Kwao. 
Abiria
 wakianza kupanda treni tayari kwa kurejea makwao mara baada ya treni la
 mwakyembe kuwasili kituoni hapo kwenye majira ya saa kumi na moja na 
dakika ishirini jana.
 Mmoja
 wa Abiria aliyegeuza na treni hilo aliyepandia Kituo cha Kamata, kwa 
lengo la kuwahi kiti akibishana na mmoja wa abiria aliyechini katika 
foleni.
Wakazi
 wa Jiji la Dar wakiwa kwenye foleni ya kupanda treni maarufu kwa jina 
la treni ya mwakyembe jana kwenye majira ya saa 11 jioni katika kituo 
cha Stesheni.
Wakazi
 wa jiji la Dar wakipanda kwenye treni la mwakyembe mara baada ya 
kuwasili kwenye kituo chake cha Stesheni jana Kwenye majira ya Saa 11 
Jioni, tayari kwa kuwarudisha majumbani kwao likitokea Mjini kuelekea 
Ubungo ambapo ndio kituo cha Mwisho.
**************************
**************************
ABIRIA
 wanaotumia usafiri wa Treni, nao wameiga staili ya abiria wa Mbagala, 
ambapo hulazimika kila jioni na asubuhi abiria katika kituo cha Treni 
cha Stesheni kupanda Treni hilo na kugeuza nalo, jambo ambalo huwafanya 
abiria wanaosubiria usafiri huo mwisho wa kituo kukosa nafasi na siti 
kutoka na treni hilo kufika kituoni likiwa tayari limejaa.
Abiria
 waliokuwa wakisubiria treni hilo walianza kulalamika baada ya kuona 
kila behewa likiwa tayari limeshajaa kabla hata treni hiyo haijafika 
kwenye kituo chake cha mwisho kwa lengo la abiria hao kuwahi . 
Baada ya Tukio hilo kutokea kulizuka sintofahamu kwa baadhi ya wafanyakazi na Askari Polisi ambao hawajawahi kuona utaratibu huo ukifanyika na kupelekea Abiria kuhisi tayari wafanyakazi wa treni hiyo waneshaanza kuchakachua kitu ambacho utaratibu hauruhusu.
Baada ya Tukio hilo kutokea kulizuka sintofahamu kwa baadhi ya wafanyakazi na Askari Polisi ambao hawajawahi kuona utaratibu huo ukifanyika na kupelekea Abiria kuhisi tayari wafanyakazi wa treni hiyo waneshaanza kuchakachua kitu ambacho utaratibu hauruhusu.
No comments :
Post a Comment