Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Friday, February 22, 2013

Skylight Band yatoa shukrani kwa mashabiki na kutambulisha nyimbo mpya ya 'Nasaka Dhoughs'





Mkurugenzi Mkuu wa Bendi ya Skylight Anneth Kushaba akizungumza na vyombo vya habari jijini Dar es Salaam jana ambapo ametoa shukurani kwa mashabiki na waandishi wa habari kwa kuiunga mkono bendi hiyo pamoja na kuwa bado ni changa. Ameongeza kuwa bendi hiyo inapiga muziki aina ya ‘Afro Pop’ kutokana na falsafa yao ya muziki na mahitaji ya soko la muziki wa ‘Live’ hapa Tanzania. Kulia ni mwanamuziki Joniko Flower.
Kushaba amewataka mashabiki wa muziki kuhudhuria kwa wingi katika show yao watakayopiga katika kiwanja chao cha nyumbani cha Thai Village kuanzia saa tatu usiku.
Mwanamuziki Joniko Flower wa Skylight Band akitoa kionjo kwa waandishi wa habari waliohudhuria hafla fupi ya kutambulisha nyimbo mpya na kuwashukuru mashabiki wao kwa kuwaunga mkono.
Aneth Kushaba AK 47 akiongoza kundi la vijana wa Skylight Band kutoa burudani wakati wakitambulisha nyimbo yao mpya ya "Nasaka Dhoughs" iliyomo kwenye albam yao yenye nyimbo nane inayokaribia kutoka hivi karibuni.
Sam Mapenzi akijimwaga na sebene la Carolina.
Mwanamuziki Sony Masamba akikamua.
Salma Yusuf uzao wa BSS akionyesha kipaji chake kwa waandishi wa habari wakati wa uzinduzi wa single mpya ya Skylight Band.
Na Mo Blog.
Kwa niaba ya bendi nzima ya Skylight Mkurugenzi Mkuu Anneth Kushaba ameomba ushirikiano kutoka kwa mashabiki, hamasa na kuungwa mkono katika kuendeleza burudani na kuleta ladha mpya ndani ya fani ya Muziki.
Pia ameomba ushirikiano kutoka kwa wadau mbalimbali ili kuendeleza juhudi za kuwahakikishia wapenzi wanaohudhuria maonyesho yao Thai Village kila Ijumaa wanapata muziki wenye kiwango bora kama unasikiliza CD.
Kushaba amesema wamefanikiwa kuboresha sauti kwa kuongeza aina ya vyombo vinavyotumika katika maonyesho ya kimataifa.

No comments :

Post a Comment