Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Sunday, July 29, 2012

Ubalozi wa UAE wafuturisha waumini Dar


UBALOZI wa Nchi ya Falme za Kiarabu, UAE nchini kupitia taasisi ya kutoa huduma za kijamii ya Khalifa Bin Zaayid Al Nahyaan, umeamua kuwafuturisha waumini wa dini ya kiislam wa Msikiti wa Al Rahman wa Dar es Salaam kwa mwezi mzima wa mfungo wa Ramadhani.
Msaada huo wa futari ulianza kutolewa tangu kuanza kwa mfungo wa mwezi huo siku 10 zilizopita na juzi mwandishi wa habari hizi alishuhudia ugawaji wake kwa waumini hao mara baada ya swala ya Magharibi iliyoswaliwa msikini hapo na kuwafanya waumini wapate fursa ya kuwa na uhakika wa kula baada ya funga zao.
Imamu wa Msikiti huo wa Al Rahman uliopo eneo la Kinondoni, Sheikh Abdullah Salim Bahssany, akiwahutubia waumini wake wakati wakigawiwa futari hiyo, alisema huo ni msaada toka ubalozi wa UAE na utakuwa ukitolewa hapo kila siku hadi mwezi mtukufu wa Ramadhani utakapomalizika mwishoni mwa mwezi ujao.
Imamu huyo aliwaambia waumini hao kuwa wale waliokuwa na shaka na kupata futari katika funga zao, waondoe hofu kwani sasa watakuwa wakipata chakula hicho, huku akiushukuru ubalozi huo kwa ukarimu iliyouonyesha kwa waumini hao.
"Jamani futari mnayokula leo imetolewa na ubalozi wa nchi za Falme za Kiarabu na msaada huu utakuwa ukitolewa kwa mwezi mzima katika mfungo huu wa Ramadhani hivyo msiwe na hofu katika funga zenu,"alisema Sheikh Bahssany.
Nao baadhi ya waumini waliofuturishwa msikiti hapo waliushukuru ubalozi huo na kuomba watu wengine wenye uwezo kuiga mfano huo wakidai mwezi huu ndio wa waumini wa kweli kuonyesha upendo, ukarimu na kuhurumiana katika kutekeleza nguzo ya nne kati ya tano za Imani za Kiislam.
"Wengine wetu tunafunga lakini hatuna hakika ya kupata futari, lakini kwa hili linalofanywa na ubalozi huu ambao hata mwaka jana walitusaidia tunashukuru na kuomba wengine wawe wanatukumbuka wanyonge kama sisi," alisema muumini mmoja aliyekataa kutajwa jina lake gazetini.
Ubalozi huo wa UAE nchini Tanzania umekuwa na desturi ya kuwafuturisha waumini wa kiislam wa baadhi ya misikini ya miji ya Tanga, Dar, Mwanza, Arusha, Lindi, Mtwara na Shinyanga kila mwaka wakati wa mfungo ambapo kwa mwaka jana ilitumia jumla ya Dola za kimarekani 80,000 kwa huduma hiyo pamoja na kulisha daku na zaka el fitr kwa waumini wasiojiweza  wa misikiti ya mikoa hiyo.

No comments :

Post a Comment