Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Wednesday, July 25, 2012

Rais Kikwete ashiriki katika mazishi ya Mzee Azzan Ally Mangushi



Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akishiriki katika mazishi ya kada wa CCM mzee Azzan Ally Mangushi yaliyofanyika katika makaburi ya Kisutu jijini Dar es Salaam leo mchana. Mzee Mangushi aliwahi pia kuwa mjumbe wa Halmashauri kuu ya CCM wilaya ya Kinondoni.

*****************************
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete mchana wa leo, Jumanne, Julai 24, 2012, ameungana na mamia ya waombolezaji katika kumzika kada maarufu wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Ndugu Azzan Ally Mangushi kwenye makaburi ya Kisutu, Dar Es Salaam.
Rais Kikwete amewasili kwenye makaburi hayo ya Kisutu, katikati ya Jiji la Dar es Salaam, kiasi cha saa saba na dakika 45 kujiunga na mamia ya waombolezaji kumzika Ndugu Mangushi ambaye alikuwa Mjumbe wa Halmashauri ya Mkoa ya Chama cha Mapinduzi.
Mbali na wananchi wa kawaida na wanachama wa CCM, mazishi hayo pia yamehudhuriwa na wanachama wa Klabu ya Soka la Simba ya Dar es Salaam ambako alikuwa mwanachama na mhamasishaji hodari.
Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu.
Dar es Salaam.
24 Julai, 2012

No comments :

Post a Comment