Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Tuesday, July 24, 2012

KAMBI YA ILALA YAENDELEA KUMFUA BONDIA IBRAHIMU CLASS KWA AJILI YA MPAMBANO WA IDI PILI



Bondia Ibrahimu Class kushoto akipambana na Yohana Robart wakati wa mazoezi yake ya kujiandaa na mpambnano wake na Simba Watundulu utakaofanyika siku ya Idi pili katika ukumbi wa Diamond Jublee.
Kocha wa Mchezo wa ngumi Kambi ya Ilala Habibu Kinyogoli katikati akiwaelekeza mabondia Yohana Robert KUSHOTO NA Ibrahimu Class jinsi ya kutupa masumbwi kwa mpizani kwa kunyoosha mkono Class anajiandaa na mpambano wake na Simba Watundulu siku ya Idi pili katika ukumbi wa Diamond Jublee jijini Dar es salaam

Na Mwandishi Wetu
KAMBI ya ngumi Ilala ipo kwenye maandalizi mazito ya kumnoa bondia Ibrahimu Class 'Ibra Mawe' anaetarajia kuzipiga na Simba Watundulu katika uzito wa KG,60 litakalofanyika siku ya Idi pili katika ukuimbi wa Diamond Jublee.
 Akizungumza mmoja wa makocha wa kambi ya ilala inayongozwa na Kocha mkongwe wa  mchezo huo Habibu Kinyogoli, Rajabu Mhamila 'Super D', amesema katika kipindi hichi cha mwezi mtukufu wa Ramadhani wanamwandaa bondia Ibrahimu Class kwa ajili  ya mpambano huo utakaofanyika siku hiyo Super D alisema wamemuandaa bondia wao kufanya vizuri ili kuweza kumzibiti  mpinzani wake kwa kuwa wanamjua uchezaji wake awapo ulingoni hivyo wanamfundisha  mbinu mpya kwa ajili ya kumkabili mpinzani wake.
Kambi hiyo ya ngumi imewataka wadau wa mchezo uho kuja kuangali mchezo mzuri wa  masumbwi utakaonyeshwa na bondia wao kutoka kambi ya ilala Ibrahimu Class anaetamba kwa jina la 'Ibra Mawe' ambaye yupo kwenye maandalizi makali chini ya makocha wake Kinyogoli na Super D kwa ajili yampambano huo na kuwataka  wapinzani wake kwa sasa wakae chonjo kwa kuwa moto umesha washwa na akuna wa  kuuzima kwa bondia huyo chipkizi na mwenye nia ya kuupaisha mchezo wa masumbwi  Kimataifa.
Mabondia hao watakuwa wakicheza katika mpambano wa utangulizi wa RAUNDI 6 uku pambano kuu ni kati ya Ramadhani Shauli wa Tanzania na Sande Kizito wa Uganda watakaopambana kugombania mkanda wa Ubingwa wa IBF Afrika

No comments :

Post a Comment