Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Monday, July 23, 2012

RAIS DK SHEIN AWAONGOZA AWAONGOZI VIONGOZI NA WANANCHI KATIKA DUA YA HITMA KUWAOMBEA WALIOKUFA KWA AJALI YA MELI




 Na Rajab Mkasaba, Ikulu Zanzibar.

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed
Shein,  leo ameungana na viongozi mbali mbali wa Kitaifa katika dua
maalum ya hitma pamoja na Sala maalum ya Maiti (Salatul Mayyit
al-ghaib), iliyosomwa huko katika msikiti Mushawar, Mwembeshauri mjini
Zanzibar.

Sala na dua hiyo ni maalum kwa ajili ya kuwaombea watu waliokufa
kutokana na ajali ya kuzama kwa meli ya MV SKAGIT,  iliyotokea hivi
karibuni wakati meli hiyo ilipokuwa inasafiri kutoka Dar-es-Salaam
kuja Zanzibar na kusababisha vifo na majeruhi kadhaa

Katika sala na dua hiyo viongozi mbali mbali wa dini, vyama na
Serikali walihudhuria akiwemo Makamu wa Rais wa Jamuhuri ya Muunganao
wa Tanzania Mhe. Dk. Mohammed Kharib Bilal, Makamu wa Pili wa Rais wa
Zanzibar Mhe. Balozi Seif Ali Idd, Rais mstaafu wa Zanzibar Mhe. Dk.
Amani Abeid Karume.

Viongozi wengine waliohudhuria ni Mufti Mkuu wa Zanzibar Sheikh Omar
Khabh, Kadhi Mkuu wa Zanzibar Sheikh Khamis Haji, Spika wa Baraza la
Wawakishi Mhe. Pandu Ameir Kificho, Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharib
Mhe. Abdalla Mwinyi Khamis, Mawaziri, Manaibu Waziri, Wabunge,
Wawakilishi, Mashekhe mbali mbali wa Zanzibar na Tanzania Bara pamoja
na wananchi na viongozi wengine.

No comments :

Post a Comment