Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Sunday, July 29, 2012

MBUNGE RITA KABATI AISAIDIA JEZI TIMU YA TASWA IRINGA




Mbunge Rita Kabati (kushoto) akimkabidhi mwenyekiti wa TASWA mkoa wa Iringa Bw.Francis Godwin seti ya jezi kwa ajili ya timu ya TASWA jana
Mbunge wa viti maalum mkoa wa Iringa Mhe. Rita Kabati (CCM) ameisaidia jezi seti moja timu ya waandishi wa habari za michezo Tanzania (TASWA) mkoa wa Iringa kama njia ya kuiunga mkono timu hiyo katika kuhamasisha michezo mkoani Iringa.

Akikabidhi msaada huo leo kwa mwenyekiti wa TASWA mkoa wa Iringa Bw.Francis Godwin ,mbunge Kabati alisema kuwa amelazimika kutoa msaada huo kama sehemu ya kuunga mkono unzishwaji wa timu hiyo .

Kwani alisema suala la michezo lime katika ilani ya uchaguzi wa CCM hivyo akiwa kama mbunge ameguswa na mkakati wa wanahabari mkoa wa Iringa katika kuhamasisha michezo na kuwa miongoni mwa wadau wa kweli wa michezo ambao wamekuwa wakiandika habari za michezo ila pia na wao wenyewe kuonyesha mfano katika michezo kwa kuwa na timu yao.

Mbunge Kabati alitoa wito kwa wabunge wengine na wadau wa michezo katika mkoa wa Iringa kujitokeza kuisaidia timu hiyo vifaa vya michezo pamoja na misaada mbali mbali pale inapohitajika ili kuiwezesha kuwa timu bora katika mkoa wa Iringa.

No comments :

Post a Comment