Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Tuesday, July 24, 2012

TIMU YA TAIFA YA OLIMPIKI YA TANZANIA YAWASILI KWENYE KIJIJI CHA MICHEZO HIYO, STRATFORD-LONDON...!!!





Timu ya Tanzania ya Olimpiki, imewasili kwenye kijiji cha michezo ya Olimpiki kilichopo Stratford, London, ikitokea kwenye mji wa Bradford. Timu hiyo ya Tanzania, iliweka kambi ya mazoezi katika Chuo Kikuu cha Bradford tangu walipowasili nchini Uingereza wiki mbili zilizopita, ikiwa tayari kuiwakilisha Taifa katika michezo hiyo ya Olimpiki 2012. Timu hiyo ilipokelewa na Balozi wa Tanzania, nchini Uingereza, Mheshimiwa Peter Kallaghe na maofisa wengine wa Ubalozi na kusindikizwa moja kwa moja kwenye kijiji cha michezo hiyo kilichopo Stratford, ikiwa tayari kwa maandalizi na ufunguzi rasmi wa michezo hiyo utakaofanyika siku ya Ijumaa 27/07/2012 hapa London.



Pichani, Balozi wa Tanzania, Mheshimiwa Peter Kallaghe akiwa pamoja na Wanamichezo hao watakaoiwakilisha Taifa mwaka huu katika Michezo hiyo ya Olimpiki nchini Uingereza.


  KILA LA KHERI TIMU YETU YA TANZANIA

No comments :

Post a Comment