Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Tuesday, July 24, 2012

MABONDIA MCHUMIATUMBO KUZIPIGA NA ZOLA D


Mtandao wa Wasanii Tanzania (SHIWATA)
Press Release
     Mabondia Alpjonce Joseph (Mchumiatumbo) na David Michael Mlope (Zola D – King) watapambana katika Tamasha la Watani wa jadi litakalofanyika katika Sikukuu ya Idd El Fitri kwenye Uwanja wa Chuo cha Bandari Temeke.
     Pambano hilo ambalo limeandaliwa na SHIWATA ili kukusanya fedha za Ujenzi wa nyumba za kisasa za gharama nafuu kwa ajili ya Wasanii, Waandishi wa Habari na Wanamichezo katika Kijiji cha Mwanzega, Mkuranga.
     Kamisheni ya Ngumi za kulipwa nchini Tanzania (TPBC) ambalo inasimamia pambano hilo la Mabondia  hawa watakaocheza katika uzani wa juu (Heavy weight) raundi nane (8) pia kutakuwa na pambano moja la utangulizi.
     Mwenyekiti wa Kamati ya Viwango vya mabondia wa kulipwa wa TPBC,  Boniface Wambura amethibitisha kuwepo kwa pambano hilo wakati wa Sikukuu za Iddi el fitri, Agosti, 2012.
     Mwenyekiti wa SHIWATA Cassim Taalib alisema pamoja na pambano hilo, kutakuwa na mechi ya mpira wa miguu kati ya Simba na Yanga (Veteran) katika Uwanja huo huo wa Chuo cha Bandari Temeke na mshindi wa mchezo huo atazawadiwa ng’ombe dume.
     Taalib alisema kwamba kikundi cha Mchiriku cha Jagwa kitatumbuiza, Roman Mg’ande wa Msondo atapigana mieleka na Lumole Matovolwa (Big na upande wa wanawake Sophia Lubuva wa Simba atapambana na Mwajuma Jimama wa Yanga huku washangiliaji wa Mpira Pesa (Simba) watapambana  katika mpira wa miguu na Watani wao wa jadi Yanga Bomba.
     Tamasha litapambwa na mechi ya Mpira wa Kikapu ya Ngongoti pamoja na mashindano ya Pikipiki ambayo yanatarajiwa kuwa kivutio kikubwa kwa watoto na wakubwa ambao siku hiyo watakuwa wakisherekea Sikukuu ya Idd el fitri baada ya kumalizika kwa mwezi wa Ramadhani, Wasanii wa Bongo Flava nao watakuwepo.
                                            Peter Mwenda
    0786/0752/0715 – 222677
          Ofisa Habari wa SHIWATA

No comments :

Post a Comment