Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Sunday, March 21, 2010

AMINA KINARA WA GOFU LUGALO INAYODHAMINIWA NA ZAIN


Mchezaji wa gofu Amina Khamis akijiandaa akipiga mpira wakati wakati wa mashindano ya gofu yaliyofanyika katika viwanja vya gofu vya Lugalo jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki. Amina aliibuka mshindi wa jumla katika mashindano hayo ambayo yanadhaminiwa na kampuni ya Zain.

Amina Khamis meibuka mshindi wa jumla katika mashindano ya gofu yaliyofanyika katika viwanja vya mchezo huo vya Lugalo jijini Dar es Salaam baada ya kupata jumla ya pointi 23.

Mashindano hayo ambayo yanafanyika kila mwisho wa wiki chini ya udhamini wa kampuni ya simu za mkononi ya Zain Tanzania yalishirikisha wachezaji katika makundi manne, akina mama, wasichana,vijana wa kiume na wazee.

Kufuatia ushindi huo Amina alijishindia zawadi mbalimbali ikiwemo kifurushi cha Zain ambacho kina fulana, begi na vifaa vingine vya michezo kutoka Kampuni ya Simu za mkononi ya Zain ambao ndiyo wadhamini wakuu wa mashindano hayo.

Akiongea baada ya kukabidhiwa zawadi zake Amina mbaye ni mchezaji chipukizi ambaye kwa sasa ni kati ya wachezaji wanaoonyesha viwango vya juu katika gofu katika klabu ya Lugalo, alisema kuwa kwa sasa matumaini yake ni kucheza kufikia katika kiwango cha kimataifa.

Alisema kuwa kinachomtia moyo yeye na vijana wenzake ni jitihada za kampuni ya Zain katika kudhamini mchezo wa gofu katika klabu ya Lugalo, hali ambayo imesaidia kuinua viwango vya gofu kwa vijana wa klabu hiyo.

Washindi wengine ni Gidion Sayore na Rapahel Letara kwa upande wa wazee,Abdala Idd kwa vijana wa kiume na Stepania Sayore kwa wanawake.Mchezaji gofu Sophia Mathiasi akipokea zawadi kutoka Zain baada ya kuibuka mshindi wa pili katika mashindano ya gofu yaliyofanyika juzi kwenye viwanja vya gofu vya Lugalo.

No comments :

Post a Comment