Timu ya wanawake wa Tanzania ya mpira wa mikono, imepewa nafasi kubwa ya kutwaa ubingwa wa michuano maalum ya Afrika mashariki na kati *Kombe la Challenge* itakayoanza kutimua vumbi lake April 29-May 5 mwaka huu huko nchini Djibouti.
Nafasi hiyo kwa timu ya Tanzania imetolewa na katibu mkuu wa Chama cha mpira wa mikono hapa nchini TAHA, Nickolaus Mihayo alipozungumza na Michezo na Times ambapo amesema mpaka sasa timu hiyo inajiandaa vyema.
Hata hivyo Mihayo amesema timu ya Tanzania itaundwa na wachezaji kutoka Tanzani bara na visiwani ambao watatangazwa hivi karibuni.
NITAENDELEA KUWEKA MAZINGIRA WEZESHI KWA WAWEKEZAJI:RC NYONGO
-
Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Mhe. Stanslaus Haroon Nyongo, amesema ataendelea
kuweka mazingira wezeshi kwa wawekezaji ili kukuza uwekezaji na uchumi wa
Mkoa wa...
1 day ago
No comments :
Post a Comment