Taarifa za kuingia kambini kwa timu hiyo, zimetolewa na katibu mkuu wa shirikisho la soka nchini TFF Fredrick Mwakalebela alipozungumza na waandishi wa habari jijini Dar es salaam.
Mwakalebela amesema kwa ujumla timu italigharimu shirikisho la soka nchini TFF shilingi million 40 katika kipindi hichi cha maandalizi mpaka siku ya mchezo dhidi ya Somalia ambao utachezwa March 28.
Aidha mwkalebela amezungumzia maamndalizi ya timu nyingione za taifa za Tanzania ambazo pia zinajiandaa na michezo yake ya kimataifa ambapo kwa upande wa timu ya taifa ya wanawake Twiga Stars inajiandaa na mchezo wake wa marejeano dhidi ya Ethiopia huku timu ya taifa ya vijana chini ya umri wa miaka 20 ambayo inajiwinda na mchezo dhidi ya timu ya taifa ya Malawi.
No comments :
Post a Comment