Timu ya soka ya taifa ya Tanzania TAIFA STARS hii leo imeingia kambini tayari kwa kuanza maandalizi ya mchezo wake wa kufuzu kucheza fainali za mataifa bingwa ya Afrika kwa wachezaji wa ndani CHAN dhidi ya timu ya taifa ya Somalia.
Taarifa za kuingia kambini kwa timu hiyo, zimetolewa na katibu mkuu wa shirikisho la soka nchini TFF Fredrick Mwakalebela alipozungumza na waandishi wa habari jijini Dar es salaam.
Mwakalebela amesema kwa ujumla timu italigharimu shirikisho la soka nchini TFF shilingi million 40 katika kipindi hichi cha maandalizi mpaka siku ya mchezo dhidi ya Somalia ambao utachezwa March 28.
Aidha mwkalebela amezungumzia maamndalizi ya timu nyingione za taifa za Tanzania ambazo pia zinajiandaa na michezo yake ya kimataifa ambapo kwa upande wa timu ya taifa ya wanawake Twiga Stars inajiandaa na mchezo wake wa marejeano dhidi ya Ethiopia huku timu ya taifa ya vijana chini ya umri wa miaka 20 ambayo inajiwinda na mchezo dhidi ya timu ya taifa ya Malawi.
BONDIA RAMADHANI MIGWENE AMUWEKEA MIKWALA ALBANO CLEMENT BAADA YA KUKIMBIWA
NA HABIBU PENGO
-
BONDIA RAMADHANI MIGWEDE baada ya kukimbiwa na mpinzani wake Habibu Pengo
aliesaini nae kuzipiga mara ya kwanza sasa amebadilishiwa mpinzani na
atacheza na...
2 years ago
No comments :
Post a Comment