Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Tuesday, March 16, 2010

TAIFA STARS IMEINGIA KAMBINI TAYARI KUIKABILI SOMALIA

Timu ya soka ya taifa ya Tanzania TAIFA STARS hii leo imeingia kambini tayari kwa kuanza maandalizi ya mchezo wake wa kufuzu kucheza fainali za mataifa bingwa ya Afrika kwa wachezaji wa ndani CHAN dhidi ya timu ya taifa ya Somalia.
Taarifa za kuingia kambini kwa timu hiyo, zimetolewa na katibu mkuu wa shirikisho la soka nchini TFF Fredrick Mwakalebela alipozungumza na waandishi wa habari jijini Dar es salaam.
Mwakalebela amesema kwa ujumla timu italigharimu shirikisho la soka nchini TFF shilingi million 40 katika kipindi hichi cha maandalizi mpaka siku ya mchezo dhidi ya Somalia ambao utachezwa March 28.
Aidha mwkalebela amezungumzia maamndalizi ya timu nyingione za taifa za Tanzania ambazo pia zinajiandaa na michezo yake ya kimataifa ambapo kwa upande wa timu ya taifa ya wanawake Twiga Stars inajiandaa na mchezo wake wa marejeano dhidi ya Ethiopia huku timu ya taifa ya vijana chini ya umri wa miaka 20 ambayo inajiwinda na mchezo dhidi ya timu ya taifa ya Malawi.

No comments :

Post a Comment