SHIRIKISHO la Mpira wa kikapu Nchini TBF kupitia katika Kamisheni ya Waamuzi imeandaa mafunzo ya Awali kwa waamuzi wa kikapu nchini inayotambuliwa na Shirikisho la kikapu la Dunia FIBA April 10 mwaka huu mkoani Arusha.
katibu Mkuu wa TBF Alexander Msoffe amesema kozi hiyo itakuwa na manufaa makubwa kwa waamnuzi wa kikapu kwani wengi hawajapata nafasi ya kupandishwa madaraja na kutambuliwa na FIBA
Ametaja mikoa inayounda kanda hiyo kuwa ni Kilimanjaro, Tanga , Manyara na wenyeji Mkoa wa Arusha mbako Mafunzo hayo yatafanyika licha ya waamuzi wengine katika mikoa mingine wanayo nafasi ya kushiriki.
Katibu Mkuu amesema Mafunzo hayo ya siku Nne yamelenga waliowahi kucheza au wanacheza kikapu na
Walimu wa ngazi zote kuanzia Shule za Msingi nawatalazimika kujigharamia.
Kufuatia hali hiyo amewatolewa wito maafisa michezo nchini kutoa ushirikiano kwa kushirikiana na makatibu wa TBF wa Mikoa kuhakikisha wanatoa washiriki kadri wawezavyo.
Msoffe amesema licha ya kutambuliwa na FIBA itawapa Fursa nzuri waamuzi wa Tanzania kutambuliwa kimataifa zaidi hivyo ni vema kuitumia badala ya kuchezesha bila kutambuliwa wakati ni waamuzi wazuri.
BONDIA RAMADHANI MIGWENE AMUWEKEA MIKWALA ALBANO CLEMENT BAADA YA KUKIMBIWA
NA HABIBU PENGO
-
BONDIA RAMADHANI MIGWEDE baada ya kukimbiwa na mpinzani wake Habibu Pengo
aliesaini nae kuzipiga mara ya kwanza sasa amebadilishiwa mpinzani na
atacheza na...
2 years ago
Mzuka mzee wa viwanja mambo yako tunayakubali, upo juu
ReplyDelete