Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Saturday, March 20, 2010

SIMBA WAREJEA TANZANIA KISHUJAA

Wachezaji wa Simba wakilakiwa na mashabiki waliyojitokeza kuwapokea katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam, mwenye begi wa kwanza ni Mohammed Banka ambaye alifunga goli la pili, na wanyuma ni Juma Jabu "JJ".

MABINGWA wa soka Tanzania Bara, Simba walimchelewesha Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Yusuph Makamba katika uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere baada ya kutaka kuwashuhudia mashujaa hao.

Simba walirejea wakitokea Zimbabwe katika mchezo wao wa Kombe la CAF dhidi ya Lengthens FC ambapo walishinda mabao 3-0 yaliyofungwa na Mussa Hassan Mgosi, Mohamed Banka na Mohamed Kijuso.
Kundi la Friends Of Simba likiwapungia mashabiki wa Simba ambao walijitokeza kuwalaki wakati wakirejea toka nchini Zimbabwe, Mwenye kanzu ni Kassim Dewji.
Mabingwa hao walipata mapokezi ya nguvu kutoka kwa wapenzi wa timu hiyo japokuwa waliwasiri majira ya saa 3 asubuhi kwa ndege ya shirika la Kenya.

Makamba ambaye alikuwa na shughuli zake uwanjani hapo lakini alipowakuta mashujaa hao wakishuka alisimama na kuanza kusalimiana na wachezaji na kuwaahidi kuwapa chakula cha mchana.
Golikipa Juma Kaseja akisalimiana na mashabiki wakati wakiwasili mapema leo toka nchini Zimbabwe.
Akizungumzia mchezo huo, Kipa wa Simba, Juma Kaseja alisema mchezo ulikuwa mgumu sana lakini kutokana na maandalizi waliyofanya ilikuwa chachu ya ushindi.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa klabu hiyo, Hassan Dalali alisema timu yake hawatabweteka na ushindi waliopata kwani wapinzani wao si wa kubeza.

Dalali ambaye alikuwa mkuu wa msafara wa Harare alisema watajipanga kuhakikisha wanaibuka na ushindi mnono katika mchezo wa marudiano utakaopigwa wiki mbili zijazo.

No comments :

Post a Comment