
Akizungumza kutoka nyumbani kwao Zambia Phiri amesema kuna masuala yamemkwamisha na pale atakapoyakamilisha ndipo atarejea nchini.
Phiri alipoulizwa lini hasa atarejea kati ya kesho Ijumaa au Jumamosi akasema atabainisha pale atakapokuwa na uhakika lakini akisema huenda kambi ya kikosi hicho ikawekwa Zanzibar kuanzia Jumatatu huku akisema hata kama angewahi kurudi programme yake isingetimia kwakuwa kuna wachezaji takribani nane wapo kwenye kikosi cha Taifa Starz kinachocheza na SOMALIA .
Wekundu hao tayari wameanza maandalizi yao bila ya Phiri wakiwa chini ya kocha msaidizi Amri Said wakianza na mazoezi ya ufukweni.
No comments :
Post a Comment