Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Sunday, March 21, 2010

TWIGA STARS HUREEEEE....YATINGA HATUA YA PILI MATAIFA YA AFRIKA (WANAWAKE)

Mshambuliaji wa timu ya soka ya Wanawake 'Twiga Stars' Esther Chabruma (kulia) akikabiliana na mabeki wa Ethiopia, Semira Kemar Aman na Beziihan Endale Alemar wakati wa mchezo wa kusaka tiketi ya kucheza fainali za Afrika uliofanyika kwenye Uwanja wa wa Uhuru jijini Dar es Salaam.

Timu ya taiafa ya wanawake Tanzania Twiga Stars imefanikiwa kutinga hatua ya pili ya michuano ya mataifa ya Afrika kwa wanawake baada ya kutoka sare ya kufungana goli 1-1 katika mchezo wa marudiano uliyochezwa Jumamosi uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam.
Twiga Stars inasonga mbele kwa jumla ya magoli 4-2 baada ya mchezo wa kwanza kushinda 3-1 walipokutana nchini Ethiopia majuma mawili yaliyopita.

Katika mchezo wa jana timu ya Twiga Stars licha ya kufanikiwa kusonga mbele lakini ilionekana kucheza mpira katika kiwango cha chini tofauti na Ethiopia ambao walikuwa wakionekana kucheza mpira wenye mipango ya kusaka ushindi.

Sasa Twiga Stars itakutana na Eritrea katika hatua ya pili ya kusaka nafasi ya kucheza mataifa ya Afrika soka la wanawake, fainali ambazo zitafanyika nchini Afrika Kusini mwaka huu.

No comments :

Post a Comment