Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Wednesday, March 24, 2010

FIFA YAIONGEZEA TANZANIA TIKETI 90 ZA KOMBE LA DUNIA

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
24/03/2010

FIFA YATOA TIKETI ZA NYONGEZA ZA KOMBE LA DUNIA 2010

TFF inapenda kuutaarifu umma wa watanzania hususan wapenzi wa mpira walioomba kununua tiketi za Kombe la Dunia kuwa shirikisho la kimataifa la mpira wa miguu, FIFA limekubali maombi ya TFF ya tiketi za nyongeza.Itakumbukwa kuwa maombi ya tiketi yalikuwa mengi kuliko idadi ya tiketi 290 ambazo Tanzania ilikuwa imetengewa na FIFA. Maombi yaliyozidi yalikuwa 450 kwa michezo tafauti. Hata hivyo maombi mengi zaidi yalikuwa katika michezo ya robo fainali, nusu fainali na fainali.

Kwa sasa tiketi za nyongeza ambazo FIFA imeipatia Tanzania ni 90 (tisini)

Tiketi zote hizo ni za mchezo namba 61 ambao ni wa nusu fainali ya kwanza itakayochezwa Cape Town kwenye uwanja wa Green Point Julai 6 2010.

Tiketi ya bei chini ni Dola za Marekani 250 na ya bei ya juu ni dola 600.

Watakaopewa kipaumbele cha kununua tiketi hizi za nyongeza ni wale ambao waliomba lakini hawakuwafanikiwa kupata tiketi katika mgawo wa awali.Baada ya hapo watafikiriwa waombaji wengine ambao watakuwa tayari kulipa.

Hivyo basi wale wote waliowasilisha maombi wanatakiwa kufika ofisi za TFF kwa ajili ya kulipia tiketi zao.

Ifahamike kuwa kama ilivyokuwa kwa tiketi zilizouzwa awali kutakuwepo ada ya asilimia kumi (10) kwa kila tiketi kwa ajili ya utawala na gharama za kutuma fedha FIFA. Malipo yote ni tasilimu katika dola za Marekani.

Mwisho wa kulipia tiketi hizi ni April 2, 2010.


Fredrick Mwakalebela
KATIBU MKUU

No comments :

Post a Comment