
Fulham, ushindi iliyoupata wa magoli 4-1 dhidi ya klabu kongwe ya Serie A, kibibi kizee cha Turin Juventus na kusonga mbele kwa jumla ya magoli 5-4, sasa itakutana na Wolfsburg, timu nyingine ambayo iliondolewa katika hatua ya mtoano ya ligi ya mabingwa.
Robo fainali zingine mbili, Hamburg ambayo uwanja wake ndiyo utakaotumika kwa fainali za mwaka huu, Hamburg Arena, watakutana na Standard Liege ya Ubelgiji, na huku klabu za Hispania zikiuana zenyewe kwa zenyewe yaani Valencia na Atletico Madrid.
Michezo ya kwanza ya robo fainali imepangwa kuanza kupingwa April 1, huku michezo ya marudiano ikipigwa April 8.
Michezo ya nusu fainali itachezwa kati ya April 22 na 29, huku fainali ikipigwa siku ya Jumatano katika uwanja wa Hamburg Arena hapo May 12.
ratiba kamili ya UEFA CUP
Fulham v Wolfsburg
Hamburg v Standard Liege
Valencia v Atletico Madrid
Benfica v Liverpool
No comments :
Post a Comment