Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Saturday, March 6, 2010

SEMUNYU NA MIKAKATI YA KUINUA KIKAPU TANZANIA

SHIRIKISHO la Mpira wa Kikapu nchini TBF katika kuhakikisha linahamasisha na kuibua vipaji vya mchezo wa mpira wa kikapu kwa watoto imeamua kushirikiana kwa karibu na vyombo vya habari nchini.
Akizungumza jijini Dar es salaam Mwenyekiti wa Kamisheni ya watoto Selemani Semunyu alisema wamefikia hatua hiyo ikiwa ni kuibua ari kwa watoto na wazazi kuwaruhusu watoto wao kushiriki Kikapu.
“ Hatutapata wachezaji wachanga kama hawatahamasishwa kwa kuangalia ligi mbalimbali Sheria na mafanikio ya ,mchezo huo kitu ambacho kinahitaji msaada mkubwa kutoka kwa waandishi wa Habari na vyombo vya habari kwa ujumla,” alisema Semunyu.
Aliongeza kuwa hatua hiyo itasaidia kuwaonyesha wachezaji ligi mbalimbali za mpira wa kikapu Duniani ikiwemo Ligi ngumu Duniani ya kikapu ya marekani National Basketball Association NBA na mbinu na hatua mbalimbali za uchezaji pamoja na mafanikio ya wachezaji mbali mbali kupitia makala zao.
Alisema miongoni mwa vyombo vya habari ambavyo tayari vimeridhia kushirikiana na TBF ni pamoja na TBC ambao wameahidi kuonyesha ligi ya NBA kwa siku ya Jumamosi au jumapili.
“ kwa mujibu wa Mazungumzo ya Makamu wa rais wa TBF Phares Magesa na Mkurugenzi wa TBC Tido Mhando kilichobaki kwetu ni kumuandaa mchambuzi ambaye atakuwa akifafanua mambo mbalimbali katika mchezo husika,”alisema Semunyu.
Semunyu alisema Mchakato unaendelea kwa vyombo vingine na pia kutafuta uwezekano wa Ligi za ndani kuonyeshwa hata kwa baadhi ya michezo.
Pia alisema anavishukuru vyombo mbalimbali vya habari nchini ambavyo viko mstari wa mbele kutangaza masuala ya kikapu hali ambayo yanaongeza chachu kwa vijana kutaka kupata mafanikio kama yaliyofikiwa kwa Hasheem Thabeet.
Aliongeza kuwa Tanzani kuna vijana wengi wenye sifa ya uchezaji kikapu kinachotakiwa sasa ni mchango wa wadau wa habari ambao tayari wengine wameonyesha ili kliniki mbalimbali za kuwabaini wachezaji zinapofanyika kutoa mwamko kwa watoto na Vijana kujitokeza.

No comments :

Post a Comment