Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Friday, March 19, 2010

TMK WADAI KUHUJIMIWA LIGI DARAJA LA KWANZA

Baada ya kubanjuliwa mabao matatu kwa moja kwenye mchezo wa ligi daraja la kwanza hatua ya tisa bora dhidi ya AFC, mmiliki wa timu ya TMK UTD Abass Mtemvu ameonyesha kuchukizwa na sababu zilizopelekea kufungwa kwa timu hiyo.
Mtemvu amelazimika kuzungumzia sababu hizo hii leo alipokutana na waandishi wa habari, kufuatia kuibuka kwa toka kwa mashabiki walioushuhudia mchezo huo ambao wamedai wenyeji AFC walipata ushindi katika hali ya ndivyo sivyo.
Amesema pamoja na hatua hiyo ya AFC kupata ushindi wa ndivyo sivyo pia viongozi wa timu ya TMK Utd walipigwa na askari jeshi waliokua wakilinda usalama kwenye uwanja wa Sheikh Amri Abeid.
Michuano hiyo imeendelea tena hii leo katika uwanja wa sheikh mari Abaeid kwa kuchezwa michezo miwili ambapo katika mchezo wa kwanza timu ya Rhino toka mkoani Morogoro ilicheza na Polisi Dodoma.
Matokeo ya mchezo huo ni kwamba maafande wa jeshi la p[olisi toka mkoani Dodoma wamefanikiwa kuchomoza na ushindi wa mabao mawili kwa sifuri.
Mchezo wa pili ulikuw akati ya timu ya Ruvu Shooting toka mkoani Pwani dhidi ya Costal Union toka mkoani Tanga.
Matokeo ni kwamba timu ya Ruvu Shooting imepata ushindi wa bao moja kwa sifuri.

No comments :

Post a Comment