Semina ya soka la wanawake iliyokuwa ikiendelea kwenye makao makuu ya shirikisho la kandanda Tanzania TFF uwanja wa karume imefikia tamati hii leo chini ya mkufunzi wa shirikisho la soka Dunia FIFA.
Akizungumza mara baada ya semina hiyo mkufunzi huyo wa FIFA MONICA STARB amesema wanawake wanaweza wakafanya vizuri katika mchezo wa soka endapop wataendelezwa.
Amesema licha ya nchi nyingi zilizoendelea haziruhusu wanawake kufanya kile wanachokipenda lakini amedai kwa kuendelea wanawake kufanya vizuri kutaendelea kufungua milango.
Ameongeza kuwa ili wanawake milango yao ya mafanikio iweze kufanikiwa wanalazimika kuyatumia vema mafunzo hayo ambayo wameyapata kwa kuinua soka la wanawake Tanzania.
Amesisitiza ni muhimu kuwepo kwa makocha wazuri wanawake lakini pia ukapewa kipaumbele mashuleni na wazazi wakahusishwa katika kuhamisisha mchezo wa soka la wanawake Tanzania.
CCM YATOA SALAMU ZA RAMBIRAMBI KWA ASKOFU MKUU RUWA’ICHI KUFUATIA KIFO CHA
KADINALI PENGO
-
Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimetoa salamu za rambirambi kwa Askofu Mkuu wa
Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Mhashamu Jude Thaddeus Ruwa’ichi
OFMCap...
12 hours ago
No comments :
Post a Comment