Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Tuesday, March 16, 2010

SIMBA WANYIMWA HOTELI ZIMBABWE

Wawakilishi pekee wa Tanzania kwenye michuano ya kimataifa wekundu wa msimbazi simba, wamewasili salama wa salamini huko mjini Harere nchini Zimbabwe tayari kwa pambano lao la mwishoni mwa juma hili dhidi ya wenyeji wao Lengthens.
Akizungumza na Michezo na Times meneja wa kikosi cha wekundu hao Inocent Njovu amesema safari yao toka nchini Tanzania ambayo ilianza majira ya alfajiri ilikuwa salama na wamewasili mjini Harare mishale ya saa saba mchana ambapo kwa ukanda wa Afrika mashariki ilikuwa mishale ya saa nane alasiri.
Njovu amesema pamoja na kuwasili salama huko mjini Harare nchini Zimbabwe, mpaka mishale ya jioni walikua bado hawajapatiwa sehemu ya malazi ambayo ilistahili kuandaliwa na wenyeji wao.
Wakati wawakilishi hao pekee wa Tanzania wakiwasili huko nchini Zimbabwe tayari kwa pambano lao la mwishoni mwa juma hili, hapa nyumbani shirikisho la soka nchini TFF kupitia kwa katibu wake mkuu Fredrick Mwakalebela limewatakiwa kheri wawakilishi hao.
Njovu amesema kiongozi wa msafara ambaye anatoka shirikisho la kandanda Tanzania TFF Msafiri Mgoi anafuatilia suala hilo la wao kuwekwa nje jambo lililowalazimu wachezaji kuacha mabegi nje ya hoteli na kwenda mazoezini huku wakiwaacha viongozi wakifuatilia mustakabali wa wapi watalala.

No comments :

Post a Comment