Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Friday, March 19, 2010

WAFAHAMU WAPINZANI WA SIMBA LEO


Klabu ya Lengthens Football Club ilianzishwa mwaka 2002 baada ya kununuliwa ikiwa daraja la pili ambapo ilikuwa ikifahamika kama Black Eagles. Lengthens Football Club – jina lake la utani ni “The Happy People” ama watu wenye furaha – ilifanikiwa kupanda kucheza ligi kuu mwaka 2007.
ikiwa ni mwaka wake wa tatu katika ligi kuu, Lengthens tayari imekwishafanikiwa kutwa ubingwa wa BancABC Sup8r.
Mwaka 2008, Lengthens ilifanikiwa kucheza fainali katika michuano hiyo lakini ilifungwa na Caps United.

Safari ya Lengthens hata hivyo imeanza mbali hata kabla ya mwaka 2002. Asili ya klabu hiyo inakumbukwa toka wakati wa ligi ya Kanda ya Kuwadzana wakati klabu hiyo ilipokuwa ikiundwa na vijana wadogo ambapo walikuwa wakicheza kama sehemu ya burudani tu.
Nje ya soka na majukumu ya kijamii, klabu hii, ilipewa jina la Young Pirates na kufanikiwa kutwaa tuzo mbali mbali. Baada ya mafanikio hayo ndipo viongozi walipoamua sasa kuitazama katika mafanikio zaidi na soka la kulipwa ambalo linaushindani zaidi na ndipo walipoamua kuiingiza katika ligi.
Viongozi wake ndipo walipoamua kuinunua klabu ya ligi daraja la pili na kufanikiwa kuipandisha daraja hadi ligi kuu mwishoni mwa msimu wa mwaka 2006.
Lengthens Football Club siku zote imekuwa ni klabu yenye mafanikio na inakumbukwa mwaka 2003 “The Happy People” walifanya vizuri kiasi cha kutamba katika michuano ya ZIFA Unity Cup.
Hata hivyo Lengthens Football Club katika michuano hiyo ilipoteza mchezo wake wa kwanza dhidi ya Dynamos.
Mwaka 2006, Lengthens ilifanikiwa kutinga hatua ya pili ya michuano ya CBZ Unity Cup baada ya kuifunga CAPS United lakini ilipoteza dhidi ya Buymore kwa mikwaju ya penati.
Mwaka 2007, Lengthens ilimaliza ikiwa miongoni mwa timu nane za juu katika ligi na mwaka uliyofuata katika michuano ya Sup8r, ambapo walipoteza mchezo dhidi ya Caps United. Mwaka 2008, Lengthens ilimaliza ikiwa miongoni mwa timu nne za juu na pia ilishiriki tena katika michuano ya Sup8r, kombe ambalo walifanikiwa kulitwaa kwa mara ya kwanza katika ligi.
Lengthens ama The Happy People inanolewa na kocha Mandla Masuku wakati meneja wa timu ni Robert Matoka. Mussa Gwasira ni raisi wa klabu na patron wa Lengthens Football Club. Mwenyekiti wa Lengthens ni Irvin Mereki wakati katibu mkuu ni John Chikochi.
Plaxedes Masenda ni shabiki nambari moja wa Lengthens Football Club.
Makocha waliyowahi kuifundisha klabu ya Lengthen FC ama “The Happy People” ni pamoja na Moses Chunga, Bigboy Mawiwi na marehemu Vusa Mlilo.
Makocha wengine ni pamoja na Gilbert Mapemba ambaye sasa anaifundisha klabu ya Caps United, Ephraim Mazarura sasa anaifundisha klabu ya Dynamos, Tendayi Nyamadzawo sasa yupo Caps United na Felix Kuswatuka ni miongoni mwa wachezaji ambao wanarekodi nzuri na kiwango cha hali ya juu ambao waliwahi kutamba na Lengthens.
Kauli mbiu ya Lengthes fc ni “If God is for us, who can be against us - The Happy People”

No comments :

Post a Comment