Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Saturday, March 13, 2010

AZAM FC KUREFUSHA SHANGWE ZA UBINGWA WA SIMBA???

Timu ya Azam FC siku ya Jumapili itashuka katika uwanja wa Uhuru kuikaribisha Simba SC katika kukamilisha mchezo wa 20 wa ligi kuu ya Vodacom.
Azam FC ikiwa na pointi 31 itakuwa na wakati mzuri wa kushinda mchezo huo ili kukaa vyema katika nafasi ya tatu ya msimamo wa ligi, huku Simba wakiwa na salio la pointi mbili kutawazwa kuwa mabingwa wapya wa ligi hiyo wanaitaji ushindi wa hali na mali.
Kocha wa Azam FC Itamar Amorin amesema kikosi chake kipo sawa kuikabili Simba SC na kutoipa nafasi ya kuwa mabingwa kupitia Azam FC.
Amesema "Simba ni timu ngumu na nzuri natarajia kikosi changu kitaleta upinzani mkubwa na kuondoka na ushindi katika mechi hiyo".Kikosi cha timu ya Azam FC kinafanya mazoezi kwa ajili ya mchezo huo katika viwanja vya Chuo kikuu cha Dar es Salaam, huku mchezaji mmoja tu Erasto Nyoni akiwa majeruhi baada ya kuumia dakika za mwanzo katika mchezo dhidi ya Yanga.
Katika mchezo wa mzunguko wa kwanza Azam FC walipoteza mchezo huo kwa kukubali kufungwa goli 1-0 katik amchezo wa tisa wa ligi uliochezwa katika uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam.
Wakati huo huo klabu ya Simba ambayo ilikuwa imeweka kambi visiwani Zanzibar imerejea leo jijini Dar es Salaam tayari kwa mchezo huo hapo kesho.
Golikipa nambari moja wa Simba Juma Kaseja amesema kwa maandalizi waliyoyafanya wanaamini kesho wanaingia uwanjani kwa lengo moja tu la kutaka kutawazwa mabingwa wapya wa ligi kuu Tanzania Bara kwa kuizaba Azam FC."kaka unakumbuka katika mzunguko wa kwanza tulitokea Zanzibar kula marashi ya karafuu tukawafunga Azam na kesho watake wasitake lazima walowe tusherehekee ubingwa bwana" anasema kaseja.
Simba ambayo inaongoza ligi kuu Tanzania Bara ikiwa na jumla ya Pointi 53 inahitaji poitni mbili tu iweze kutangaza ubingwa.

No comments :

Post a Comment