Kutoka
Kushoto: Mkuu wa Wilaya ya Nyang'hwale, Ibrahim Marwa, Mkuu wa Wilaya
ya Kahama, Benson Mpesya wakipokea msaada wa sehemu ya tani 200 za
mahindi kutoka kwa Meneja Mkuu wa Mgodi wa Dhahabu wa Bulyanhulu,
Dennis Hoof (wa pili kulia)na Makamu wa Rais wa African Barrick Gold
(ABG),Utekelezaji Muundo, Peter Gereta katika hafla iliyofanyika katika
Kata ya bulyanhulu wilayani Kahama mkoa wa Shinyanga hivi karibuni.
Maeneo yatakayonufaika na msaada huo uliogharimu kiasi cha milioni 163/-
ni kwa wale waliokumbwa na uhaba wa chakula katika vijiji 14 vilivyoko
Bugarama, Mwingiro na Bulyanhulu wilaya ya Kahama mkoa wa Shinyanga na
Nyang'hwale Mkoa mpya wa Geita.
Mkuu
wa Wilaya ya Kahama, Benson Mpesya akipokea msaada wa tani 200 za
mahindi kutoka kwa Meneja Mkuu wa Mgodi wa Dhahabu wa Bulyanhulu, Dennis
Hoof (wa pili kulia). Kushoto ni Diwani wa Kata ya Bulyanhulu, Joseph
Makoba.
Mkuu wa Wilaya ya Nyang'hwale, Ibrahim Marwa akihutubia kabla ya makabidhiano.
Mkuu
wa Wilaya ya Kahama, Benson Mpesya akihutubia kabla ya makabidhiano.
Kulia ni Meneja Mkuu wa Mgodi wa Dhahabu wa Bulyanhulu, Dennis Hoof na
Kushoto ni Diwani wa Kata ya Bulyanhulu, Joseph Makoba na Mkuu wa
Wilaya ya Nyang'hwale, Ibrahim Marwa.
Mbunge
wa Msalala, Ezekiel Maige akibadilishana mawazo na Meneja Mkuu wa
Mgodi wa Dhahabu wa Bulyanhulu, Dennis Hoof (katikati), na Makamu wa
Rais wa African Barrick Gold (ABG),Utekelezaji Muundo, Peter Gereta.
Meneja Mkuu wa Mgodi wa Dhahabu wa Bulyanhulu, Dennis Hoof akijadiliana jambo na Mkuu wa Wilaya ya Kahama, Benson Mpesya.
Kutoka
Kushoto: Meneja Mkuu wa Mgodi wa Dhahabu wa Bulyanhulu, Dennis Hoof ,
Mkuu wa Wilaya ya Kahama, Benson Mpesya na Mkuu wa Wilaya ya
Nyang'hwale, Ibrahim Marwa wakikagua sehemu ya shehena ya mahindi mara
baada ya makabidhiano.
Sehemu ya viongozi wa vijiji lengwa na msaada huo waliohudhuria hafla hiyo.Picha Zote na Badi John
No comments :
Post a Comment