Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Monday, July 9, 2012

ROBO FAINALI COPA COCA-COLA 2012




Robo Fainali ya michuano ya Copa Coca-Cola 2012 inayokutanisha vijana wenye umri chini ya miaka 17 inaanza kesho (Julai 10 mwaka huu) kwa timu nne kuumana kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume, Dar es Salam.


Temeke na Mjini Magharibi ndizo zitakazocheza robo fainali ya kwanza kuanzia saa 2.30 asubuhi. Mara iliyoivua ubingwa Kigoma itacheza robo fainali ya pili dhidi ya Morogoro kwenye uwanja huo huo.

Robo Fainali ya tatu itachezwa keshokutwa (Julai 11 mwaka huu) kwa kuzikutanisha timu za Kinondoni na Mwanza. Mechi hiyo itaanza saa 2.30 asubuhi na kufuatiwa na nyingine kati ya Dodoma na Tanga itakayoanza 10 kamili jioni.

Nusu fainali ya michuano hiyo iliyoanza Juni 24 mwaka huu katika mikoa ya Dar es Salaam na Pwani ikishirikisha timu 28 itafanyika Julai 13 mwaka huu kwenye uwanja huo huo.

Mshindi wa mechi kati ya Temeke na Mjini Magharibi, na Kinondoni dhidi ya Mwanza ndiyo watakaocheza nusu fainali ya kwanza. Nusu fainali ya pili itakuwa mshindi wa mechi ya Mara na Morogoro dhidi ya mshindi wa mechi ya Dodoma na Tanga.

Fainali itafanyika Jumapili (Julai 15 mwaka huu). Mechi zote kuanzia hatua ya robo fainali hadi fainali zitafanyika kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume.

No comments :

Post a Comment