Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Thursday, August 16, 2012

RAFAEL NADAL AJITOA MICHUANO YA WAZI YA MAREKANI 'US OPEN 2012'



M
NEW YORK, Marekani
 MCHEZA Tenisi mahiri Rafael Nadal, amelazimika kujitoa kwenye Mashindano ya Wazi ya Marekani (US Open) yanayotarajia kuanza mwishoni mwa mwezi huu, kutokana na jeraha la goti linaloendelea kumtesa.
Nadal, 26, nyota huyo wa kimataifa wa Hispania, pia alishindwa kuwa sehemu ya washiriki wa mashindano ya Olimpiki jijini London iliyofikia tamati hivi karibuni kwa tatizo hilo na hajacheza michuano yoyote tangu alioposhiriki Wimbledon.
Nyota huyo anayeshika nafasi ya tatu ya viwango vya ubora wa mchezo huo duniani, ambaye alishinda Grand Slams jijini New York mwaka 2010, pia alishindwa kucheza Masters Series huko Toronto na Cincinnati, lakini sasa ana matumaini ya kucheza Flushing Meadows.
Nadal alisema: “Ninasikitika sana kutangaza rasmi kwamba, bado siko tayari kucheza tenisi na hivyo nalazimika kujitoa katika Mashindano ya Wazi ya Marekani yatakayofanyika kuanzia Agosti 27, jijini New York mwaka huu.
“Nasikitika kuwa nitaendelea kukosa kucheza mashindano makubwa yenye uungwaji mkono mkubwa, lakini naendelea na maandalizi ya kuhakikisha narudi vema mchezoni nikiwa kwenye hali stahili.
“Napenda kusema shukrani kwa mashabiki wangu wote, hasa wa mashindano ya New Yorke. Nitawakosa kwa mwaka huu wa mashindano hayo ya wazi!”
Mkurugenzi wa Mashindano ya US Open, David Brewer aliongeza: “Rafael amewasiliana nasi kututaaruifu kuwa hayuko fiti kushindana katika mashindano ya mwaka huu na kwamba ameamua kujitoa katika michuano hiyo.
“Tuna matumaini makubwa ya kumuona akirejea tena viwanjani na kumuona akiangalia mbele zaidi kuelekea mashindano ya mwakani ya US Open hapa New York."
Mashindano ya US Open yanatarajia kuanza kutimua vumbi hapo Agosti 27, huku wakali kama Roger Federer na Novak Djokovic wakiwa miongoni mwa nyota wa kiume watakachuana, wakati David Ferrer akitarajiwa kupanda hadi nafasi za juu.

No comments :

Post a Comment